Tanzania yapaa matibabu ya moyo kimataifa


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akikata utepe wakati wa uzinduzi wa kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Oysterbay lililopo Oyster plaza Haile Salassie barabara ya Ali Bin Said leo jijini Dar es Salaam.

Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akimuelezea Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama huduma inayotolewa na kitengo cha Lishe kwa wagonjwa wa moyo wakati wa uzinduzi wa kliniki mpya ya Taasisi hiyo iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza daktari bingwa wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Smita Bhalia wakati wa uzinduzi wa Kliniki ya Oysterba leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwajulia hali wagonjwa waliofika kutibiwa katika kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Kawe alipotembelea Kliniki hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza mgonjwa aliyefika kutibiwa katika kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Kawe alipotembelea kliniki hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea duka la dawa lililopo katika kliniki ya JKCI Kawe leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wadau wa afya wakati wa uzinduzi wa kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea mafanikio ya taasisi hiyo wakati wa uzinduzi wa kliniki mpya ya taasisi hiyo iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya mabalozi na viongozi mbalimbali wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakiendelea wakati wa uzinduzi wa kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama wakati wa uzinduzi wa kliniki ya JKCI iliyopo Oysterbay leo jijini Dar es Salaam.

Na: JKCI

**************************************************************************************************************

Tanzania kuwa miongoni mwa mataifa yanayoongoza barani Afrika katika kutoa huduma za matibabu ya kibingwa hususani matibabu ya moyo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ufunguzi wa Kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Oyster plaza Haile Salassie barabara ya Ali Bin Said leo jijini Dar es Salaam.

Mhe. Muhagama alisema Serikali imeendelea kufanya jitihada za uwekezaji katika sekta ya afya lengo likiwa kukabiliana na vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo.

“Kadiri siku zinavyozidi kwenda serikali imeendelea kuwekeza kwenye vifaa tiba na vifaa vya uchunguzi lakini haijasahau kuendelea kuwekeza kwenye ubingwa na ubobezi kwa wataalamu wetu ili tuweze kuendelea kutoa huduma kwa wananchi wanaotuamini”,

Mhe. Mhagama alisema Kliniki ya Oystebay si tu itahudumia wageni wanaotoka  nje ya nchi lakini pia ni eneo ambalo linaweza kufikika kirahisi na watanzania wanaoishi katika maeneo haya.

“Leo nimeweza kutembelea pia kliniki ya JKCI iliyopo Kawe na kukuta wananchi wengi wanapata huduma pale ambao wameishukuru sana Serikali kwa kuwapunguzia adha ya kufuata huduma mbali”, alisema Mhe. Jenista

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt Peter Kisenge aliesema JKCI imetumia zaidi ya bilioni 2.2 kuwekeza katika kliniki ya Oysterbay na Kliniki ya Kawe.

Dkt. Kisenge alisema vifaa vilivyopo katika kliniki hizo ni vya hali ya juu, pamoja na mashine ambazo zinatumia akili bandia kwa ajili ya kugundua tatizo alilonalo mgonjwa

“Kliniki yetu inatoa huduma za matibabu kupitia huduma mtandao (Tele consultation) ambapo hata kama ukiwa nje ya Tanzania unaweza kupata huduma kutoka kwa daktari wetu yeyote”,

Moja ya vitu vikubwa ambavyo vinaweza kuitambulisha taaasisi yetu kwa upekee ni pamoja na kufanya upasuaji wa kubadilisha valvu ya moyo bila kufungua kifua (TAVI Procedure) huu ni utaalamu wa hali ya juu”, alisema Dkt. Kisenge 

Dkt. Kisenge alisema Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inaenda kuikomboa Afrika katika masuala ya moyo kwani nchi za Zambia, Malawi, Comoro na Kongo sasa zimeanza kuitumia kwaajili ya kuzijengea uwezo.

 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa