JKCI yapongezwa kwa kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo barani Afrika

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nicole Kanyawa akimwelezea huduma zinazotolewa na taasisi hiyo Msanii wa Muziki nchini Mrisho Mpoto atembelea banda la Taasisi hiyo lililiokuwa katika mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Benjamini akimuelezea namna moyo unavyofanya kazi mshiriki wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika kutoka nchini Malawi alipotembelea banda la Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nicole Kanyawa akimuelezea namna taasisi hiyo inavyofanya utalii tiba mshiriki wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika kutoka nchini Djibouti alipotembelea banda la taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Daktari kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika Nelly Iteba akizungumza na wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhusu masuala ya tiba utalii alipotembelea banda la JKCI wakati wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika.


Balozi wa Tanzania Nchini Zambia Lt. Gen. Mathew Mkingule akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika.

Na: JKCI

*****************************************************************************************************************************

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imepongezwa kwa kuwa moja ya taasisi zinazotoa huduma ya matibabu bingwa bobezi ya moyo katika bara la Afrika na kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda nje ya bara la Afrika kufuata huduma hizo.

Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni na washiriki wa mkutano wa nishati wa wakuu wa nchi za Afrika uliomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam waliotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Akizungumza wakati alipotembelea banda hilo raia wa Djibouti Raclud Abdilz alisema moja ya kitu alichojifunza hapa nchini ni pamoja na uwepo wa Taasisi hiyo ya kibingwa inayotoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo kwa watu kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

“Nimefurahishwa na taarifa za taasisi hii kwani sikuwa naifahamu, sasa waafrika tunaweza kupata huduma ndani ya bara letu na karibu na nchi zetu tofauti na kuzifuata mbali na nchi zetu”, alisema Raclud.

Naye Salu Omari kutoka nchini Malawi aliipongeza Taasisi hiyo kwakuwa na ushirikiano mzuri na nchi ya Malawi kwani sasa wananchi wa Malawi wanapata huduma JKCI.

“Mmekuwa mkija nchini Malawi kutuletea huduma zenu, leo nimefika hapa Tanzania na kuona ambavyo nchi yenu imewekeza katika matibabu haya ya moyo”, alisema Salu.

Taasisi hiyo inapokea  wagonjwa kutoka nchi  za Somalia, Malawi, Kenya, Rwanda, Visiwa vya Comoro, Msumbiji, Nigeria, Siera Leone, Zimbabwe, Uganda, Zambia, Congo, Ethiopia, Burundi nan chi zingine za nje ya bara la Afrika zikiwemo za  Armenia, China, Ujerumani, India, Norway, Ufaransa, Uingereza na Marekani. 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa