Prof. Kabudi; Watanzania jivunieni kuwa na JKCI, Ni Taasisi ya umahiri Barani Afrika
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Profesa Palamagamba
Kabudi akipimwa joto la mwili na Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Jackline Mwaipopo alipotembelea katika banda la JKCI wakati wa maonesho
ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika
viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini
Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Profesa Palamagamba
Kabudi akimsikiliza Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Emmanuel Lingido alipotembelea banda la JKCI wakati wa maonesho ya 50 ya
Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja
vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es
Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Profesa Palamagamba
Kabudi akipokea zawadi kutoka kwa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce alipotembelea banda la JKCI wakati
wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA)
yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara
ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Afisa Uuguzi wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimuonesho Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Profesa Palamagamba Kabudi betri
ya moyo (Pace maker) alipotembelea banda la JKCI wakati wa maonesho ya 50 ya
Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja
vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es
Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Profesa Palamagamba
Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na
wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wanaoshiriki katika
maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA)
yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo
barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
***********************************************************************************************
Watanzania wametakiwa
kujivunia uwepo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwani ni taasisi ya
umahiri katika Bara la Afrika inayotoa huduma za kisasa za uchunguzi na
matibabu ya magonjwa ya moyo kwa viwango vya kimataifa.
Wito huo umetolewa leo na
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Prof.
Palamagamba Kabudi alipotembelea banda la JKCI katika Maonesho ya 50 ya
Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) ambapo aliwataka watanzania
kuitumia taasisi hiyo na kuiunga mkono hususan katika kampeni yake ya
kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo ili waweze kupata matibabu na
kuendelea kutimiza ndoto zao.
Prof. Kabudi
aliipongeza JKCI kwa huduma zake za kisasa za tiba ya moyo, akisema
ameridhishwa na kiwango cha utaalamu alichokiona pamoja na uwepo wa wataalamu
wabobezi wanaotoa huduma na elimu kwa wananchi katika maonesho hayo hatua
ambayo inaonesha dhamira ya taasisi hiyo ya kuwafikia watanzania popote walipo
na kuwapatia huduma za kibingwa.
Aidha Prof. Kabudi alizitaka
hospitali nyingine nchini kuiga kampeni ya “Jua Namba Zako” ambayo inalenga
kuwahamasisha wananchi kufahamu viashiria muhimu vya afya zao ili kusaidia
kinga na utambuzi wa mapema wa magonjwa ya moyo na magonjwa mengine
yasiyoambukiza.
Prof. Kabudi
alisisitiza kuwa huduma zinazotolewa na JKCI ni za kiwango cha juu na
zinawafikia watanzania wa makundi yote bila ubaguzi hivyo kuimarisha afya ya
jamii na kuongeza uelewa kuhusu kinga na matibabu ya magonjwa ya moyo.





Comments
Post a Comment