Posts

Showing posts from April, 2023

Kambi ya matibabu ya moyo yaokoa milioni 493

Image
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Africa  la nchini Marekani kumfanyia  upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo  wa Cath lab mgonjwa mwenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo leo jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 15 wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wamepatiwa matibabu katika kambi hiyo. Wataalamu wa afya ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Cardiography - ECHO) mgonjwa ambaye ana matatizo za mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo leo jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 15 wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wamepatiwa matibabu katika kambi hiyo. Wataalamu wa afya ya Taasisi Ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiandaa vifaa kwa ajili ya kumfanyia upasuaji wa moyo ...

Wagonjwa 10 kutibiwa mfumo wa umeme wa moyo

Image
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Africa  la nchini Marekani kumfanyia  upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo  wa Cath lab mgonjwa mwenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo leo jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 10 wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi hiyo. Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiangalia umeme wa moyo unaoingia kwa mgonjwa unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya CRTD Programmer  wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo leo jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 3 kati ya 10 wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wameshafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo. ********************************************************************************************************

Dkt. Kisenge aishukuru Israel kwa kutoa huduma za matibabu kwa watoto

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Naibu Mtendaji Mkuu Hospitali ya King Faisal ya nchini Rwanda Frederic Ngirabacu wakionesha mkataba wa kutibu wagonjwa wa moyo na kuwajengea uwezo wa kuwatibu wagonjwa wa moyo wataalamu wa afya wa Hospitali hiyo. Mkataba huo umesainiwa jana jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Save a Child’s Heart – SACH la nchini Israel Simon Fisher. ************************************************************************************************************************** Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge amelishukuru Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart – SACH) la nchini Israel kwa kuendelea kutoa huduma za upatikanaji wa matibabu ya moyo na ujuzi kwa nchi mbalimbali za Afrika. Akizungumza baada ya kusaini mikataba ya miaka mitatu wa makubaliano na Hospitali ya King Fa...

JKCI yasaini mkataba wa kutibu wagonjwa wa moyo wa Zambia na Rwanda

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia Dkt. Shumba Chabwela wakisaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu wa kutibu wagonjwa wa moyo wa nchini Zambia na kuwajengea uwezo wataalamu wa afya wa hospitali  hiyo wa jinsi ya kuwatibu wagonjwa wa moyo. Mkataba huo umesainiwa  leo jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakipongezana na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia Dkt. Shumba Chabwela mara baada ya kusaini mkataba wa kutibu wagonjwa wa moyo na kuwajengea uwezo wa kuwatibu wagonjwa wa moyo wataalamu wa afya wa hospitali hiyo. Mkataba huo umesainiwa  leo jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kise...

Wahitimu mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa mahututi na dharura

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi Afisa Uuguzi Uwicyeza Allen kutoka Hospitali ya King Faisal iliyopo jijini Kigali nchini Rwanda cheti cha kuhitimu mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa mahututi na dharura. Kozi hiyo ya miezi sita ilihudhuriwa na washiriki   22 kutoka nchini Rwanda na Hospitali mbalimbali za hapa nchini. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi Afisa Uuguzi Danny Hakorimana kutoka Hospitali ya King Faisal iliyopo jijini Kigali nchini Rwanda cheti cha kuhitimu mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa mahututi na dharura . Kozi hiyo ya miezi sita ilihudhuriwa na washiriki  22 kutoka nchini Rwanda na Hospitali mbalimbali za hapa nchini. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi Afisa Uuguzi Masoud Mheruka kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) iliyopo jijini Dodoma cheti cha ku...

Wapewa mafunzo ya kujikinga na kudhibiti maambukizi

Image
Mwezeshaji wa mafunzo ya mpangilio maalum katika mazingira ya kazi (5’S) pamoja na kukinga na kudhibiti maambukizi (IPC) Valentina Msechu akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kutekeleza majukumu yao kwa kufuata 5’S ili kuleta tija ndani ya kazi za kila siku wakati wa mafunzo hayo ya siku tatu yanayotolewa katika Ukumbi wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edward Msukwa akichangia hoja wakati wa mafunzo ya siku tatu kuhusu mpangilio maalum katika mazingira ya kazi (5’S) pamoja na kukinga na kudhibiti maambukizi (IPC) yanayotolewa kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam Afisa kumbukumbu za afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vedastus Lazaro akielezea namna ambavyo kitengo cha kumbukumbu za afya kinavyofanya kazi wakati wa mafunzo ya siku tatu kuhusu mpangilio maalum katika mazingira ya kazi (5’S) pamoja na kukinga na kudhibiti maambukizi (IPC) yanayotolewa kwa wafanyakazi wa Taas...

Watu 601 wapimwa moyo Iringa

Image

Watu 601 wapimwa moyo Iringa

Image
Fundi sanifu wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gerson Mpondo akimfanyia mgonjwa kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku tano iliyomalizika leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH). Mtafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zabella Mkojera akimsikiliza mkazi wa Iringa Sifael Kivamba wakati akimfanyia utafiti wa ufahamu wa magonjwa ya moyo kabla ya kufanyiwa vipimo vya moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akimpima mzinguko wa tumbo mkazi wa Iringa kabla ya kufanyiwa vipimo vya moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) Na: JKCI ******************************************************************************************************************** Jumla ya watu...

Wataalam wa JKCI wawafundisha wataalam wa Chato jinsi ya kutumia mashine ya Ventilator

Image
Daktari Bingwa wa Usingizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Faraji Lydenge na Afisa Uuguzi wa JKCI Ally Athuman wakiwafundisha wataalam wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda chato (CZRH) na Hospitali ya Wilaya ya Chato namna ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyotolewa na wataalam wa JKCI katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato.   Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) Dkt. Brian Mawala akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) yaliyofanywa na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kumalizika hivi karibuni. Daktari bingwa wa wagonjwa mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akiwafundi wataalam wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda chato (CZRH) na Hospitali ya Wilaya ya Chato namna ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) kabla ya kuanza mafunzo kwa vitend...

Dkt. Kisenge: Fanyeni kazi kwa ushirikiano ili kuleta ufanisi kazini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa chama cha wafanyakazi, madaktari na wafamasia tawi la JKCI uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi, madaktari na wafamasia Taifa Dkt. Samuel Rweyemamu akizungumza na wanachama wa chama hicho tawi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Katibu wa chama cha wafanyakazi, madaktari na wafamasia tawi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. George Longopa akizungumza na wajumbe wa mkutano huo    wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. *********************************************************************************************************************************...

Iringa washukuru kupata huduma za matibabu ya moyo

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Epheta Edward akimpima wingi wa sukari mwilini mkazi wa Iringa Magreth Sanga wakati wa kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya moyo inayofanywa na wataalam wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa. Daktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) Regina Kipemba akishirikiana na Fundi sanifu wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gerson Mpondo kumfanyia mwananchi kipimo cha kuangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiography – ECG) wakati wa kambi maalum ya siku tano inayofanywa na wataalam kutoka JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa IRRH. Mtafiti wa Taasisi ya Moyo jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimuuliza maswali ya ufahamu kuhusu magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo mkazi wa Iringa Christina Chibona kabla ya kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mk...

Madaktari bingwa wa moyo wapiga kambi Iringa

Image

Iringa kufaidika na huduma za matibabu ya moyo

Image
Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akizungumza na wakazi wa Iringa kuhusu mfumo bora wa maisha wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari bingwa wa moyo kutoka JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH). Kambi hiyo ya siku tano itamalizika siku ya ijumaa 7 Aprili 2023  Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimsomea majibu mkazi wa Iringa Sulle Ayubu mara baada ya kufanya vipimo vya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magreth Ng’ondya akimwelezea mkazi wa Iringa Lucas Ngailo umuhimu wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza wakati wa kambi maalum ya siku tano inayofanywa na wataalam kutoka JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) Baadhi ya wananchi wa Iringa wakiwa katika foleni y...

Kambi maalum ya uchunguzi na matibabu ya moyo yafanyika Iringa

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Elizabeth Meli akimpima shinikizo la damu mwilini (BP) raia wa Switzerland Lans Sottwals aliyefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) leo kwa ajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayofanywa na wataalam hao kwa kushirikiana na wenzao wa IRRH. Mtafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Loveness Mfanga akimfanyia utafiti mwananchi aliyefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) kwa ajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo leo wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo inayoendelea katika Hospitali hiyo. Kambi hiyo ya siku tano inafanywa na madaktari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa IRRH Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Janeth Mmari akimwelezea mwananchi wa Iringa Imelda Harrison namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo alipofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) kwa ajili ya kupata huduma za uchu...