Wataalam wa JKCI wawafundisha wataalam wa Chato jinsi ya kutumia mashine ya Ventilator

Daktari Bingwa wa Usingizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Faraji Lydenge na Afisa Uuguzi wa JKCI Ally Athuman wakiwafundisha wataalam wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda chato (CZRH) na Hospitali ya Wilaya ya Chato namna ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyotolewa na wataalam wa JKCI katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato.
 

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) Dkt. Brian Mawala akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) yaliyofanywa na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kumalizika hivi karibuni.


Daktari bingwa wa wagonjwa mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akiwafundi wataalam wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda chato (CZRH) na Hospitali ya Wilaya ya Chato namna ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) kabla ya kuanza mafunzo kwa vitendo wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyotolewa na wataalam wa JKCI katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato.  

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) Dkt. Brian Mawala akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator) yaliyofanywa na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kumalizika hivi karibuni.

**************************************************************************************************************************


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa