Iringa kufaidika na huduma za matibabu ya moyo

Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akizungumza na wakazi wa Iringa kuhusu mfumo bora wa maisha wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari bingwa wa moyo kutoka JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH). Kambi hiyo ya siku tano itamalizika siku ya ijumaa 7 Aprili 2023 

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimsomea majibu mkazi wa Iringa Sulle Ayubu mara baada ya kufanya vipimo vya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magreth Ng’ondya akimwelezea mkazi wa Iringa Lucas Ngailo umuhimu wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza wakati wa kambi maalum ya siku tano inayofanywa na wataalam kutoka JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH)


Baadhi ya wananchi wa Iringa wakiwa katika foleni ya kupatiwa huduma wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku tano inayofanywa na madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH)

Na: JKCI

*************************************************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa