Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) atembelea banda la JKCI katika maonesho ya SABASABA
Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo akipokea zawadi kutoka
kwa daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Thabit Ramadhani alipotembelea kliniki ya Taasisi hiyo iliyopo katika maonesho
ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika
viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini
Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
***********************************************************************************************



Comments
Post a Comment