Posts

Showing posts from July, 2020

Wananchi wameshauriwa kujenga tabia ya kupima afya zao mara kwa mara na kuwa na bima ya afya ambayo itawasaidia pindi watakapouguwa

Image
Wataalamu wa magonjwa wa moyo wakiangalia maendeleo ya aliyekuwa Mbunge wa Nzega Mhe. Lucas Lumambo Selelii aliyefanyiwa upasuaji mkubwa wa kusimamisha moyo na kupandikiza mshipa wa damu kwenye moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rosemary Mpella akimpima shinikizo la damu mwilini (BP) aliyekuwa Mbunge wa Nzega Mhe. Lucas Lumambo Selelii aliyefanyiwa upasuaji mkubwa wa kusimamisha moyo na kupandikiza mshipa wa damu kwenye moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Wananchi wameshauriwa kujenga tabia ya kupima afya zao mara kwa mara kwa kufanya hivyo watatambua kama wana maradhi au la na kama wana maradhi wataweza kupata huduma za matibabu kwa wakati. Pia wameombwa kuwa na bima ya afya ambazo zitawasaidia kupata matibabu pindi watakapouguwa kwani maradhi huja muda wowote, wakati wowote na mahala popote bila ya kupiga hodi. Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na aliyekuwa Mbunge wa Nzega Mhe. L

Shiriki CRDB Bank Marathon kwa ajili ya kuchangisha fedha za matibabu ya moyo kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza kuhusu asilimia kubwa ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo kusumbuliwa na  magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo wakati wa mkutano wa waandishi wa habari  uliofanyika leo jijini Dar es Salaam uliohusu mbio za CRDB Bank Marathon. Viongozi wa Taasisi mbalimbali ambazo zitashiriki katika mbio za CRDB Bank Marathon wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB   Abdulmajid  Nsekela mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa waandishi wa habari uliohusu mbio hizo ambazo lengo lake ni  kuchangisha fedha za matibabu ya moyo kwa watoto wanaotoka katika familia zisizo na uwezo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Viongozi wa Taasisi mbalimbali ambazo zitashiriki katika mbio za CRDB Bank Marathon wakiwa katika picha ya pamoja  mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa waandishi wa habari uliohusu mbio hizo ambazo lengo lake ni  kuchangisha fedha za matibabu ya moyo

WATAALAM WABOBEZI WA MOYO WAPANDIKIZA KIFAA CHA KUUSAIDIA MOYO KUFANYA KAZI VIZURI BILA KUTUMIA MTAMBO WA CATHLAB

Image
Kwa mara ya kwanza wataalamu wabobezi wa moyo na wazibuaji wa mishipa ya damu ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamepandikiza kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Pacemaker) nje ya Taasisi hiyo bila ya kutumia mtambo wa Cathlab. Mgonjwa aliyewekewa pacemaker alipata ajali iliyosababisha uti wa mgongo  kupata shida na kusababisha baadhi ya viungo vya mwili kupoteza  uwezo wa kufanya kazi ikiwemo mishipa ya damu  inayoratibu uwezo wa moyo kutengeneza mapigo yake (Sympathetic Waves System). Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaama daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Yona Gandye alisema kutoka na tatizo alilolipata mgonjwa mara baada ya kupata ajali  mapigo ya moyo yalishuka hadi kufikia 30 kwa dakika na mgonjwa kuonesha   dalili za ukosefu wa mahitaji muhimu ya mwili  yanayosambazwa na mapigo ya moyo ambayo  ni oxygen , virutubisho, madini na chakula. “Mgonjwa huyo alikuwa amelazwa katika Taasisi ya M

*Watanzania washauriwa kulinda afya zao kufurahia ‘matunda’ Uchumi wa Kati*

Image
KULINDA afya kwa kuzingatia mtindo bora wa maisha, ulaji unaofaa, kufanya mazoezi, kuchunguza afya mara kwa mara na kuepukana na mtindo usiofaa wa maisha, ni siri pekee itakayowawezesha Watanzania kufurahia ‘matunda’ Tanzania kuingia nchi zenye Uchumi wa Kati. Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni  na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Prof. Mohamed Janabi alipozungumza na waandishi wa habari , katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (SABASABA) na kusisitiza kwamba ni wajibu wa kila mmoja kuendelea kulinda afya yake. “Nilipoona nchi yetu imeingia Uchumi wa Kati, nilifurahia sana lakini baadae nikakaa na  kujiuliza, maana yake ni kwamba wananchi watakuwa na hela nyingi zaidi na wataishi maisha marefu zaidi. “Inabidi kama nchi tuanze kuwatayarisha sasa hivi kwa kuwaelimisha jinsi ya kuishi maisha bora wakiwa na afya bora, kwa sababu kwa kutokufanya hivyo, tutajikuta wananchi watakuwa na hela nyingi lakini wakazitumia kwa muda mfupi

Nafasi ya mwanamke katika magonjwa ya moyo

Image

MFANYAKAZI BORA ROBO YA NNE YA MWAKA WA FEDHA 2019/2020 APONGEZWA

Image
Mfanyakazi bora robo ya nne ya mwaka wa fedha 2019/2020 Dkt. Smita Bhalia akipokea Tuzo ya mfanyakazi bora kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati wa hafla fupi ya kumpongeza leo Jijini Dar es Salaam

BILIONEA SANINIU LAIZER ATEMBELEA BANDA LA JKCI NA KUVUTIWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA KATIKA BANDA HILO

Image
Mtaalam wa maabara kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jesca Mlay akimweleza Bilionea Saniniu Laizer namna ambavyo maabara ndogo iliyopo katika banda la JKCI inavyotoa huduma ya kuchunguza vipimo vya damu vilivyotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo alipotembelea banda la JKCI wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa leo Jijini Dar es Salaam Daktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimwelezea Bilionea Saniniu Laizer namna ambavyo wananchi wamekua na mwitikio mkubwa wa kufanya uchunguzi wa afya ya moyo katika banda la JKCI alipotembelea banda hilo kuona huduma zinazotolewa wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa leo Jijini Dar es Salaam. Bilionea Saniniu Laizer aipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa huduma za ushauri na upimaji wa magonjwa ya moyo wanazozitoa kwa wananchi wanaotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Sal

WALIOTIBIWA MOYO NJE YA NCHI ‘WAKIMBILIA’ BANDA LA JKCI -SABASABA

Image
Fundi Sanifu wa Moyo (Cardiovasicular technologist) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abubakar Dalidali akimpima urefu, uzito na uwiano wa urefu na uzito (BMI) mwananchi alietembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naizihijwa Majani akimpima mwananchi alietembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume shinikizo la damu (BP) pamoja na kutoa ushauri wa magonjwa ya moyo wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Wagonjwa saba waliowahi kwenda kufanyiwa upasuaji wa moyo nje ya nchi ambao hawajaweza kurudi huko kuhudhuria kliniki zao, ‘wamekimbilia’ katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), lililopo kwenye maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa -SABASABA. Katika banda la JKCI wameweza kuonwa na wataalamu wabobezi wa magonjwa ya moyo na kisha kupatiwa utaratibu

MAANDALIZI HUDUMA MPYA KUTIBU MFUMO WA UMEME WA MOYO ‘MBIONI’ KUKAMILIKA

Image
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regina Hess akifuatilia huduma zinazotolewa katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda hilo wakati wa maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Kushoto ni Daktari kutoka JKCI Pedro Pallangyo. Daktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimwelezea Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bernard Konga mwitikio wa wananchi kufanya uchunguzi wa afya ya mioyo yao katika banda la JKCI wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Huduma mpya kabisa ya kutibu tatizo la mfumo wa umeme ulioharibika kwa njia ya kisasa zaidi inatarajiwa kuanza kutolewa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), kati ya kipindi cha kuanzia mwezi Agosti hadi Oktoba, mwaka huu. JKCI hivi sasa ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ili kuanza kutoa huduma hiyo baada ya kupatiwa na Serikali kiasi cha Sh. bil 4.3 kwa ajili ya kusimika mitambo pamoja na

WANANCHI WAVUTIWA NA MASHINE YA VENTILATOR ILIYOKO BANDA LA JKCI

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mary Haule akiwaelezea wananchi namna ambavyo mashine ya kusaidia kupumua (ventilator) inavyotumika kwa wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Wataalam wa maabara kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakipima vipimo vya damu kwa ajili ya kuangalia magonjwa ya moyo kwa wananchi waliofika katika banda hilo kwa ajili ya kupima afya zao wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Wananchi waliotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika Maonesho ya Sabasaba wamevutiwa na uwepo wa chumba cha mfano cha kuhudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) pamoja na mashine maalum ya kupumulia ‘ventilator’. Mashine hiyo ndiyo ambayo hutumika kusaidia mgonjwa mwenye shida ya upumuaji kuweza kupumua vema baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa ikiwemo upasuaji wa moyo. Mkazi wa Buguru

ASILIMIA 68 WAKUTWA NA UZITO ULIOPITILIZA

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimpima mwananchi alietembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume shinikizo la damu (BP) pamoja na kutoa ushauri wa magonjwa ya moyo wakati wa Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) George Msabila akielezea vifaa mbalimbali vinavyotumika katika chumba cha upasuaji mdogo wa moyo kwa wananchi waliotembelea banda la JKCI katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mary Haule akimpima kiwango cha sukari mwilini  mwananchi aliyetembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume wakati wa  maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwapima wananchi waliotembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume shinikizo la damu (BP) pamoja na kutoa ushauri wa magonjwa ya moyo waka

TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) YAOMBWA KUWAFIKIA WANANCHI WENGI ZAIDI HASA WANAOISHI MAENEO YA VIJIJINI

Image
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwapima wananchi waliotembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume shinikizo la damu (BP) pamoja na kutoa ushauri wa magonjwa ya moyo wakati wa maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mary Haule akimpima kiwango cha sukari mwilini   mwananchi aliyetembelea banda la JKCI JKCI lililopo ukumbi wa Karume wakati wa   maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Smitha Bhalia akimweleza kuhusu ugonjwa wa kutanuka kwa moyo mwananchi aliyetembelea banda la JKCI lililopo ukumbi wa Karume wakati wa   maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.   Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Winnie Masakuya akimuelezea mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo   namna ambavyo mishipa   inayopeleka damu kwenye moyo inavyoweza ku