TAARIFA KWA UMMA
TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE KUTOA HUDUMA KWA WANANCHI
WAKATI WA MAONESHO YA SABASABA
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuwajulisha
wananchi kuwa inashiriki maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es
Salaam yanayofanyika katika Uwanja wa Maonyesho wa Biashara wa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere uliopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe
01/07/2020 hadi tarehe 13/07/2020.
Wananchi wote wa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na mikoa ya jirani
mnakaribishwa kutembelea Banda letu lililopo ukumbi wa Karume ili muweze kupata huduma mbalimbali
zinazohusiana na afya ya Moyo.
Madaktari wetu bingwa wa magonjwa ya moyo chini ya uongozi wa Prof.
Mohamed Janabi watakuwepo katika banda
letu kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.
“Tunajali Afya yako”.
Imetolewa na:
Anna Nkinda
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
01/07/2020
Comments
Post a Comment