Huduma za ushauri, upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo zatolewa kwenye banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika maonesho ya Sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam
Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimwonesha
kifaa kisaidizi cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Pacemaker) mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona
huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.
Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwahudumia
wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupima magonjwa ya moyo
wakati wa maonesho ya 45 ya Kimataifa ya biashara ya Dar es Salaam yanayofanyika
katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa.
Wafamasia wa kampuni ya kuagiza na kusambaza dawa za binadamu
ya Salama Pharmaceuticals Limited wakimpatia dawa za moyo bila malipo yoyote
yale mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupima magonjwa ya moyo.
Mteknolojia wa maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Jordan Megabe akimchukuwa vipimo vya damu mwananchi
aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupimwa vipimo vya magonjwa ya moyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimsikiliza Mfamasia wa kampuni ya kuagiza
na kusambaza dawa za binadamu ya Salama Pharmaceuticals Limited Maila Kazoya alipokuwa
akimweleza aina za dawa wanazozitoa bila
malipo kwa wananchi wanaokutwa na
matatizo ya moyo mara baada ya kupimwa na kukutwa na matatizo hayo na wataalamu
wa JKCI.
Baadhi ya washiriki wa maonesho ya 45 ya Kimataifa ya
biashara ya Dar es Salaam kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na Julius Charles aliyetembelea banda la Taasisi
hiyo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.
Comments
Post a Comment