Posts

Showing posts from August, 2021

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Image
Muonekano wa chumba cha ICU leo tarehe 26 Agosti 2021  

Wasiochanjwa chanjo hatarini zaidi damu kuganja wakiugua UVIKO - 19

Image

Fanyeni kazi kwa uweledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yenu ya kazi

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akimkabidhi cheti cha pongezi mstaafu ambaye alikuwa Afisa Uuguzi wa JKCI Marcelina Granima wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu iliyofanyika katika ukumbi wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Na: JKCI Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa kufanya kazi kwa uweledi, ufanisi na kuepuka vitendo vyote vinavyoweza kuwasababishia kushindwa kufikia hatua ya kustaafu katika utumishi wa umma. Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu wawili waliofikia ukomo wa utumishi wa umma hivi karibuni na kuagwa leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Akizungumza wakati wa hafla hiyo Dkt. Waane amesema kuwa wapo watu wengi ambao wanaanza utumishi wa umma katika ngazi mbalimbali lakini hawafikii ukomo wa utumishi wao kutokana na sababu mbalimbali, hivyo ni vyema kwa

Wafanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/21 wapongezwa

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akimkabidhi zawadi ya ngao mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya kwanza Mary Haule wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo.  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya pili Fredy Tupa wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa robo ya nne  ya  mwaka wa fedha 2020/2021 aliyeshika nafasi ya tatu Ashura Ally wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi bora watatu iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa f

JKCI yafikisha elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 kwa Wafanyakazi wa TICTS

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS baada ya kualikwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutoa elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 pamoja na kutoa chanjo kwa wafanyakazi hao Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam Baadhi ya wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS wakisikiliza elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi (hayupo pichani) kabla ya kutoa chanjo ya UVIKO – 19 kwa wafanyakazi hao Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam Afisa Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Patrick Agustino akiwasajili katika mfumo wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS kwa ajili ya kupata chanjo ya UVIKO – 19 iliyokuwa inatolewa na wataalam wa afya kutoka JKCI Jan

Viongozi na watu maarufu wachanja chanjo ya UVIKO - 19 wakati wa mbio za CRDB Marathon

Image
  Afisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Janeth Haulle akimsajiri mwananchi aliyetembelea banda la JKCI kwa ajili ya kuchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 baada ya kumalizika kwa mbio za CRDB Marathoni zilizofanyika katika viwanjwa vya Farasi Oystebay leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto 100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Oliver Marandu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 Mtanzania aliyewahi kushiriki shindano la Big Brother Afrika 2003 Mwisho Mwampamba baada ya kumalizika kwa mbio za CRDB Marathoni zilizofanyika katika viwanjwa vya Farasi Oystebay leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Oliver Marandu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mhanga wa kwanza wa kurona nchini Tanzania Isabella Mwampamba baada ya kumalizika kw

CRDB MARATHON YACHANGIA MILIONI 200 KWA AJILI YA MATIBABU YA WATOTO 100 WENYE MAGONJWA YA MOYO WANAOTIBIWA JKCI

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiwaongoza viongozi wengine katika matembezi ya kilometa 5 wakati wa mbio za CRDB Marathon kuchangia matibabu ya watoto 100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI leo Jijini Dar es Salaam  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akirishiki mazoezi ya viungo mara maada ya kumalizika kwa mbio za CRDB Marathon zilizofanyika katika Viwanja vya Farasi Oyster bay leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchangia watoto 100 wenye magonjwa ya Moyo wanaotibiwa JKCI Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza wakati wa mbio za CRDB Marathon kuchangia watoto 100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI zilizofanyika katika Viwanja vya Oyster bay leo Jijini Dar es Salaam Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi hundi ya sh

Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete watakiwa kufanya kazi kwa kufuata maadili na kuepuka mazingira ya rushwa

Image
  Mkurugenzi wa utawala na Fedha wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA Agnes Kuhenga akisoma bajeti ya Taasisi hiyo kwa mwaka wa  fedha 2021/22 wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa  kutoa huduma  kwa wateja wanaowahudumia kwa   kufuata maadili ya kazi   na kuepuka mazingira ya rushwa kwa kufanya hivyo wananchi wataridhika na huduma wanazozitoa. Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi wakati  akizungumza na wajumbe waliohudhuria kikao cha  baraza la wafanyakazi wa Taasisi hiyo. Prof. Janabi ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI  alisema ushirikiano wa pamoja baina ya wafanyakazi pamoja na uwazi katika utendaji kazi vinachangia kwa kiasi kikubwa kutoa huduma bora kwa wateja wanaowahudumia wakiwemo wagonjwa. "Unapomuhudumia mteja toa huduma yako kwa moyo  na kujituma  epuka kuchukuwa he

Wachezaji wa Mpira wa Miguu kutoka Klabu za Yanga, Simba, Azam na Simba Queens wachoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO - 19

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akitoa elimu kuhusu chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kabla ya chanjo hiyo kuanza kutolewa kwa wachezaji wa klabu za Yanga, Simba na Azam. Baadhi ya wachezaji wa mpira wa miguu kutoka klabu ya Simba wakifuatilia elimu kuhusu chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 iliyokua ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kabla ya chanjo hiyo kuanza kutolewa kwa wachezaji hao leo Jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Oliver Marandu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mchezaji wa mpira wa miguu kutoka klabu ya Yanga Abdallah Shaibu (Ninja) baada ya wachezaji wa klabu hiyo kufika katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kuchoma chanjo Mchezaji wa mpira wa miguu kutoka klabu ya Simba Queens Aisha Juma akichoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Ki

Viongozi wa Serikali, Wafanyakazi wa sekta ya Afya na Wananchi waendelea kuchomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19 inayotolewa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Image
Balozi Mteule Togolani Mavura akichanjwa  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 inayotolewa  katika Taasisi ya Moyo Jakaya ikwete (JKCI)  iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea umuhimu wa kuchanja  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kabla ya chanjo hiyo kuanza kutolewa kwa viongozi wa Serikali, wananchi pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo. Mkurugenzi wa Kurugenzi  ya  Uuguzi ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akitoa maelekezo ya namna watakavyochanja  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kwa wananchi waliokuwa wanasubiri kuchanja chanjo hiyo. Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho akichomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Afisa  Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joshua Ogutu akimchoma   chanjo ya  kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mwananchi aliyefika JKCI kwa ajili ya kuchoma chanjo hiyo