CRDB MARATHON YACHANGIA MILIONI 200 KWA AJILI YA MATIBABU YA WATOTO 100 WENYE MAGONJWA YA MOYO WANAOTIBIWA JKCI
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza wakati wa mbio za CRDB Marathon kuchangia watoto 100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI zilizofanyika katika Viwanja vya Oyster bay leo Jijini Dar es Salaam
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi hundi ya shilingi milioni 200 iliyotolewa leo katika Viwanja vya Farasi Oyster bay Jijini Dar es Salaam na Benki ya CRDB zilizokusanywa kutoka kwa washiriki wa mbio za CRDB Marathon kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto 100 wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Hii ni mara ya pili kwa Benki hiyo kuratibu mbio za CRDB Marathon kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI
Picha
na: JKCI
Comments
Post a Comment