JKCI yafikisha elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 kwa Wafanyakazi wa TICTS

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS baada ya kualikwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutoa elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 pamoja na kutoa chanjo kwa wafanyakazi hao Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS wakisikiliza elimu ya chanjo ya UVIKO – 19 iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi (hayupo pichani) kabla ya kutoa chanjo ya UVIKO – 19 kwa wafanyakazi hao Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam

Afisa Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Patrick Agustino akiwasajili katika mfumo wafanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS kwa ajili ya kupata chanjo ya UVIKO – 19 iliyokuwa inatolewa na wataalam wa afya kutoka JKCI Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joshua Ogutu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mfanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joshua Ogutu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mfanyakazi wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam

Na: JKCI

Wafanyakazi wa kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services – TICTS wameishukuru Serikali ya awamu ya sita pamoja na watendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kuwathamini na kuwafuata maala pa kazi kwa ajili ya kutoa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19

Wakizungumza wakati wa zoezi la kutoa chanjo ya UVIKO – 19 lililofanyika Jana katika ofisi za TICTS zilizopo Kurasini Jijini Dar es Salaam wafanyakazi hao wamesema kuwa kutokana na ratiba ngumu waliyonayo katika kutekeleza majukumu yao ingekuwa ngumu kwao kupata elimu sahihi ya chanjo ya UVIKO -19 pamoja na kupata chanjo kama wataalam kutoka JKCI wakiongozwa na Prof. Mohamed Janabi wasingefika katika eneo lao la kazi na kuwapatia fursa ya kuchanja chanjo hiyo kwa hiari.

Akizungumza na waandishi wa habari, mfanyakazi wa TICTS Rose Kalima amesema kuwa baada ya kupata hamasa kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa hiari yake alitamani kupata chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 lakini kutokana na ratiba za kazi kumbana hakuweza kwenda kuchanja hadi wataalam wa JKCI walipofika katika ofisi za TICTS.

“Nimefurahi leo nimepata chanjo ya UVIKO – 19 kwa urahisi bila ya kuangaika kwenda kuitafuta, elimu tuliyoipata leo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Janabi pia imetupa hamasa kubwa kujitokeza mbele kuchanja, Wito wangu kwa wanawake waache kusikiliza maneno ya mtaani yanayopotosha kuusu chanjo, ingekuwa na madhara kama ambavyo tunadanganyana mtaani wataalamu wangetuambia maana sisi ndio mama na dada zao hivyo sidhani kama mtu angeweza kumuangamiza mama ama dada yake” alisema Rose.

Kwa upande wake Revokatus Deus ambaye pia ni mfanyakazi wa TICTS ameushukuru uongozi wa TICTS pamoja na JKCI kwa kuwapa wafanyakazi wa TICTS nafasi ya pekee kupata elimu inayoonyesha faida nyingi za kuchanja chanjo kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19.

“Sikutegemea kama ipo siku hata sisi huku tungefikiwa na wataalamu hawa kutupa elimu inayoweza kumbadilisha mtu kutoka katika mawazo hasi na kuwa balozi mzuri katika jamii inayonizunguka, nimepata elimu sahihi ya chanjo ya UVIKO – 19, faida ni nyingi zaidi kuliko hasara, watanzania endeleeni kuchanja chanjo kwani afya yako ni mtaji wako” alisema Revokatus

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania International Container Terminal Services – TICTS Hui Horace amewataka wafanyakazi wa TICTS kuendelea kuchukua taadhari zilizowekwa na Serikali dhidi ya ugonjwa wa UVIKO – 19 ikiwemo kuvaa barakoa, kunawa mikono na maji safi na tiririka, pamoja na kuchanja kwa hiari ili kuweza kuwakinga wengine pamoja na kuwa na afya bora.

“Mimi pia ni muhanga wa ugonjwa wa UVIKO – 19, ndio maana najilinda na kuwalinda nyie kwani mna wajibu katika familia zenu hivyo jilindeni ili familia zenu ziendelee kuwa na furaha” alimema Hui

 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari