Viongozi wa Serikali, Wafanyakazi wa sekta ya Afya na Wananchi waendelea kuchomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19 inayotolewa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

Balozi Mteule Togolani Mavura akichanjwa  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 inayotolewa  katika Taasisi ya Moyo Jakaya ikwete (JKCI)  iliyopo jijini Dar es Salaam.



Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea umuhimu wa kuchanja  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kabla ya chanjo hiyo kuanza kutolewa kwa viongozi wa Serikali, wananchi pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo.

Mkurugenzi wa Kurugenzi  ya  Uuguzi ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akitoa maelekezo ya namna watakavyochanja  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kwa wananchi waliokuwa wanasubiri kuchanja chanjo hiyo.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho akichomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Afisa  Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joshua Ogutu akimchoma   chanjo ya  kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 mwananchi aliyefika JKCI kwa ajili ya kuchoma chanjo hiyo.

Afisa Uuguzi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Oliver Marandu akimchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19 mwananchi aliyefika katika  Taasisi hiyo kwa ajili ya kuchoma chanjo. 

Afisa  Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joshua Ogutu akiandaa sindano yenye  chanjo ya  kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 kwa ajili ya kumchoma mfanyakazi wa Taasisi hiyo. 

Mwananchi akimuuliza swali Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi  kama mama anayenyonyesha  anaweza kuchomwa  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19.

Mkazi wa jijini Dar es Salaam akimuuliza swali Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi  kama mgonjwa wa kansa anaweza kuchomwa  chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19.



Afisa Uuguzi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) George Msabila akiwaandikia wananchi  vyeti  vya uthibitisho wa chanjo mara baada ya kuchomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 inayotolewa  katika Taasisi hiyo  iliyopo jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rydness Mlashani akiwaandikisha wananchi katika daftari la kujisajili kwa ajili ya kuchoma kuchoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 inayotolewa  katika Taasisi hiyo  iliyopo jijini Dar es Salaam. 

Afisa Uuguzi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gudila Swai akiwaandikia wananchi  vyeti  vya uthibitisho wa chanjo mara baada ya kuchomwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO – 19 inayotolewa  katika Taasisi hiyo  iliyopo jijini Dar es Salaam. 

Afisa Uuguzi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Oliver Marandu akitoa maelekezo kabla ya kuwachoma chanjo ya kuzuia maambukizi ya UVIKO -19 wananchi waliofika  katika  Taasisi hiyo kwa ajili ya kuchoma chanjo.


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari