Posts

Showing posts from July, 2022

Waziri Ummy azindua Kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao kwa watumishi wa afya kuhusu ugonjwa wa Uviko - 19

Image
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Mhe. Donald Wright, Mkurugenzi wa Shirika la kudhibiti na kukinga magojwa (US Centers for Disease Centrol and Prevention - CDC), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof. Lawrence Museru wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa Kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao kuhusu ugonjwa wa Uviko – 19 kwa watumishi wa Afya (Extension of Community Health and Care Outreach – ECHO) leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam. Kituo hicho kimeanzishwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la CDC.  Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wataalam wa afya wanaoendesha kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao kuhusu ugonjwa wa Uviko – 19 kwa watumishi wa afya wakati wa uzinduzi wa Kituo hicho uliofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Shirika la kudhibiti na kukinga magojwa ya (US Centers ...

Wafanyakazi bora robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022 wapongezwa

Image
Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya kwanza Dkt. Stella Mongela akipokea ngao ya mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya pili Faith Temba akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2021/2022 aliyeshika nafasi ya tatu Dkt. Alex Loth akipokea cheti cha mfanyakazi bora kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo wakati wa ha...

Wajumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchi hiyo watembelea JKCI kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa

Image
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akiwaeleza wajumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) jinsi huduma za matibabu ya moyo zinavyotolewa katika Taasisi    hiyo wakati wajumbe hao walipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo   akizungumza na ujumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchini humo walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya   moyo zinazotolewa. Kushoto ni Mfamasia kutoka Bohari ya Dawa (MSD) Faith Edwin. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo   akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo na ujumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchini humo mara baada ya kumaliza ziara ya...

Wauguzi kuweni marafiki wazuri wa ndugu wa wagonjwa mnaowahudumia

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo    akifunga mafunzo ya wiki 27 ya jinsi wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi (Critical Care Emergence) yaliyotolewa kwa wauguzi kutoka hospitali mbalimbali nchini. Mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na wauguzi 13 yamefungwa leo jijini Dar es Salaam. Mkuu wa kitengo cha Utafiti na Mafunzo cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.Peter Kisenge akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya wiki 27 ya jinsi wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi (Critical Care Emergence) ambao ni  wauguzi kutoka hospitali mbalimbali nchini wakati wa ufungaji wa kozi hiyo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya  akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya wiki 27 ya jinsi wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi (Critical Care Emergence) ambao ni  wauguzi kutoka hospitali mbalimbali nchini wakati wa ufungaji wa kozi...

Serikali yanunua mashine za kisasa za ECHO zinazotumika katika Hospitali za Kanda na Rufaa

Image
Mtaalam kutoka kampuni ya General Electric (GE) Judith Nyamboga akiwapa maelekezo madaktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), hospitali za Kanda Mbeya, KCMC, Bugando, Benjamini Mkapa na hospitali za Rufaa Mtwara na Chato namna ya kutumia mashine ya Echocardiogram – ECHO inazotumika kuchunguza jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika JKCI kwa madaktari hao baada ya mashine za kisasa za ECHO kununuliwa na Serikali na kupelekwa katika hospitali hizo kwaajili ya kutoa huduma kwa wagonjwa. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mayala akiwaongoza madaktari wenzake kutoka hospitali za Kanda Mbeya, KCMC, Bugando, Benjamini Mkapa na Hospitali za Rufaa Mtwara na Chato kufanya kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram – ECHO wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika katika Taasisi hiyo kwa madaktari hao baada ya Serikali kununua mashine za kisasa za ECHO ambazo z...

Wanachama wa JKCI SACCOS watakiwa kuweka akiba na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima

Image
 Mwenyekiti wa Bodi ya SACCOS ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tulizo Shem akizungumza na wanachama wa SACCOS hiyo wakati wa kikao cha kwanza kujadili bajeti kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Ushirika Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Donard Kibuti akiwaelezea wanachama wa SACCOS ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete namna ambavyo fedha wanazoweka katika SACCOS yao zinavyoweza kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja wakati wa kikao cha kwanza cha SACCOS hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wanachama wa SACCOS ya Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) wakifuatilia taarifa zilizokuwa zikitolewa katika kikao cha kwanza cha kujadili bajeti ya SACCOS hiyo kilichofanyika jana katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. Afisa Ushirika Ofisi ya Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Oliver Kaiza akiwaeleza wanachama wa SACCOS ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) umuhimu wa kuwa na leseni wakati wa kikao...

Wafurahia elimu ya lishe na mfumo bora wa maisha

Image

Wachezaji wa Simba na Yanga wakutana JKCI kwaajili ya kupima vipimo vya moyo na damu

Image
 Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mayala akimpima mchezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Simba kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wachezaji wa timu hiyo walipofika JKCI kwaajili ya kupima vipimo mbalimbali vya moyo na damu. Timu hiyo inatarajia kushiriki mashindano ya kimataifa na wachezaji wake wanafanya vipimo hivyo ikiwa ni mojawapo ya kutekeleza sheria ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwa kila mchezaji anayeshiriki mashindano hayo kupima.  Fundi sanifu wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gerson Mpondo akiwaelezea wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Simba namna kipimo cha kuangalia mfumo wa umeme wa moyo kinavyofanyika wakati wachezaji hao walipofika JKCI kwa ajili ya kupima vipimo mbalimbali vya moyo na damu. Timu hiyo inatarajia kushiriki mashindano ya kimataifa na wachezaji wake wanafanya vipimo hivyo ikiwa ni mojawapo ya kutekeleza sheria ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afri...

Wizara ya Afya yakagua utoaji huduma JKCI

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia ni mkurugenzi wa kurugenzi ya Tiba Shirikishi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delila Kimambo akiwa katika picha ya pamoja na waratibu wa huduma za matibabu kutoka wizara ya Afya na wafanyakazi wa Taasisi hiyo mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukaguzi wa kuangalia namna ambavyo hospitali za Serikali zinavyotoa huduma za matibabu lililofanywa na wataalamu kutoka wizara hiyo. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia ni mkurugenzi wa kurugenzi ya Tiba Shirikishi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delila Kimambo akizungumza na  mratibu wa huduma za matibabu kutoka wizara ya Afya Dkt. John Mwombeki mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukaguzi wa kuangalia namna ambavyo hospitali za Serikali zinavyotoa huduma za matibabu lililofanywa na wataalamu kutoka wizara hiyo.   Mkurugenzi wa Kurugenzi ya magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na   mratibu wa hudu...

wataalam 20 kutoka Taasisi ya Moyo ya Uganda wajifunza utoaji wa huduma ...

Image

Huduma za kibingwa za matibabu ya moyo zasogezwa kwa wananchi

Image

Taasisi ya JAI yasherehekea sikukuu ya Eid al-adha na wagonjwa waliolazwa JKCI

Image
Baadhi ya wawakilishi kutoka Taasisi inayojihusisha na kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) wakiongozwa na mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mwidini Athumani (mwenye koti jeusi) kushusha chakula, maji na juisi kwa ajili ya kuwapatia wagonjwa waliolazwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha sikukuu ya Eid al-adha leo katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam Mjumbe kutoka Taasisi inayojihusisha na kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) Said Khamisi akimpatia chakula mgonjwa aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Joyce Tufanyenini ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha sikukuu ya Eid al-adha leo katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam Mjumbe kutoka Taasisi inayojihusisha na kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) Said Khamisi akishirikiana na Muuguzi Kiongozi wa zamu Prisca Kiyuka kumpatia chakula na juisi mgonjwa aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakay...