Serikali yanunua mashine za kisasa za ECHO zinazotumika katika Hospitali za Kanda na Rufaa

Mtaalam kutoka kampuni ya General Electric (GE) Judith Nyamboga akiwapa maelekezo madaktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), hospitali za Kanda Mbeya, KCMC, Bugando, Benjamini Mkapa na hospitali za Rufaa Mtwara na Chato namna ya kutumia mashine ya Echocardiogram – ECHO inazotumika kuchunguza jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika JKCI kwa madaktari hao baada ya mashine za kisasa za ECHO kununuliwa na Serikali na kupelekwa katika hospitali hizo kwaajili ya kutoa huduma kwa wagonjwa.


Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mayala akiwaongoza madaktari wenzake kutoka hospitali za Kanda Mbeya, KCMC, Bugando, Benjamini Mkapa na Hospitali za Rufaa Mtwara na Chato kufanya kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram – ECHO wakati wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika katika Taasisi hiyo kwa madaktari hao baada ya Serikali kununua mashine za kisasa za ECHO ambazo zimepelekwa katika hospitali hizo kwaajili ya kutoa huduma kwa wagonjwa.


Picha na: Genofeva Matemu

***************************************************************************************


Comments

Popular posts from this blog

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi

Kutoka miaka 22 hadi kustaafu: Safari ya Lemmah yatoa somo kwa Watumishi wa Umma