Tumieni maonesho ya Sabasaba kupima magonjwa ya Moyo

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zenais Ngowi akiwaelezea wananchi namna ambavyo mashine ya kusaidia kupumua (ventilator) inavyotumika kwa wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) wakati wa maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa.


Mhasibu wa Taasisi Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Isimbula akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwa wananchi waliotembelea banda la JKCI lililopo katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupata huduma za vipimo vya magonjwa ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo

Mtafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Maklina Komba akimfanyia usajili mwananchi aliyefika katika banda la JKCI lililopo katika maonesho ya Sababasa Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupata huduma za vipimo vya magonjwa ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anastazia Moshi akimpima shinikizo la damu (BP) mwananchi aliyetembelea banda la JKCI leo lililopo katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo katika barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupata huduma za vipimo vya magonjwa ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo.

Mteknolojia wa maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jordan Megabe akimwambia namna vipimo alivyoandikiwa na daktari vitakavyofanyika katika maabara mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupimwa vipimo vya magonjwa ya moyo na kisukari wakati wa maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimsikiliza mwananchi aliyefika katika banda hilo kwa ajili ya kufanya vipimo vya magonjwa ya moyo na kisukari wakati wa maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa.


Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magreth Ng’ondya akimsomea majibu mwananchi aliyefika katika banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma ya vipimo vya magonjwa ya moyo wakati wa maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa.


 Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akitoa ushauri wa lishe kwa wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo na kisukari wakati wa maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Dar es Salaam katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa


*****************************************************************************************************

Wananchi wajitokeza kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo na kisukari katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete na kuvutiwa na huduma zinazotolewa.

Uchunguzi huo unafanyika katika Banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete lililopo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza alipotembelea banda la JKCI Mkazi wa Kisutu Jijini Dar es Salaam Mama Shainul Fernandis alisema kuwa amefika katika banda la JKCI na kupata fursa ya kuulizwa maswali kuangalia elimu aliyonayo kuhusu magonjwa ya kisukari, shinikizo la damu, kiharusi na moyo magwojwa ambayo kwa kiingereza wanaita silent killer hivyo baada ya kuangalia uwelewa wake na kupata nafasi ya kupima sukari mwilini, shinikizo la damu na vipimo vya moyo.

“Nashukuru baada ya vipimo nimepata ushauri wa kuwa napima sukari yangu mara kwa mara kwani wameona sukari yangu imeanza kuwa juu, pia watoa huduma niliowakuta katika banda la JKCI walikua wavumilivu kutusikiliza na kutusaidia jambo ambalo linatoa motisha kwetu kuwa huru kujieleza kwa uhuru”,

“Sabasaba mbali na watu kuja kutembea, kuona wanyama na kufanya manunuzi ya vitu ni vyema pia kutembelea mabanda haya yanayotoa huduma za kuchunguza afya ili kujua afya zetu, Sikutegemea kama nikija kwenye maonesho haya nitapata nafasi hii ya kuchunguza afya yangu”, alisema Mama Shainul

Aidha Mama Shainul alitoa wito kwa wananchi kuwa na tabia ya kuchunguza afya mara kwa mara kwani mazoea ya kusubiri hadi kuumwa ndio mtu achunguze afya yake huwaza kusababisha gharama za kulitatua tatizo hilo kuwa kubwa zaidi tofauti na kama matibabu yangefanyika wakati wa awali kabla ya tatizo kuwa kubwa.

Naye mkazi wa Gongo la Mboto Salehe Kipanga alisema kuwa baada ya Kutembelea banda la JKCI na kufanyiwa uchunguzi aligundulika kuwa na tatizo la sukari na shinikizo la damu hivyo kuhamashishwa kufanya na vipimo vya moyo ambavyo kwa hapo Sabasaba vinafanyika kwa bei nafuu.

“kwa kweli Taasisi hii inayojishughulisha na utoaji wa huduma za matibabu ya moyo inahitaji pongezi, wametufanyia vipimo vya moyo kwa bei nafuu sana tofauti na kama ningeenda katika hospitali zinazotoa huduma hii.

Shinikizo langu la damu halikuwa vizuri sana lakini daktari kanishauri nisitumie dawa kwanza bali nifuatilie ikiwezekana kila siku kwa kupima hadi hapo itakapoonekana nahitaji kutumia dawa ndio nitumie dawa, kwa upande wa sukari mwilini  nimepatiwa dawa ambazo nitaenda kuzitumia na kufuatilia muenendo wa sukari mwilini kwani kwa kufanya hivyo nitaweza kuepuka athari zinazotokana na magonjwa haya.

Abdalla Sidick Mkazi wa Temeke Anasema kuwa hii ni mara yake ya kwanza kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo toka kuzaliwa kwake jambo ambalo hakuwahi kufikiria kama angefanya.

“Sasa nina miaka 42 na leo nimepata fursa hii ya kuujua moyo wangu, nimefurahi sana kukuta niko salama na elimu niliyoipata hapa nitaifanyia kazi ili moyo wangu uendelee kuwa salama siku zote kwani magonjwa haya yasiyo ambukiza ni hatari”,

“Wito wangu kwa vijana ambao umri umeanza kusogea ni vizuri tukachunguza afya zetu, tukabadili mifumo yetu ya maisha ili tunapoelekea kwenye umri wa utu uzima tusipate changamoto za magonjwa yasiyoambukiza kama ugonjwa wa moyo na kuzipa gharama familia zetu kwani magonjwa haya yanahitaji fedha nyingi kuyatibu”, alisema Sidick


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)