Wajumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchi hiyo watembelea JKCI kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa


Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akiwaeleza wajumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) jinsi huduma za matibabu ya moyo zinavyotolewa katika Taasisi  hiyo wakati wajumbe hao walipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo  akizungumza na ujumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchini humo walipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya  moyo zinazotolewa. Kushoto ni Mfamasia kutoka Bohari ya Dawa (MSD) Faith Edwin.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo  akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo na ujumbe kutoka Bohari ya Dawa Msumbiji (CMAM) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (ANARME) ya nchini humo mara baada ya kumaliza ziara yao leo ya kutembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya  moyo zinazotolewa.

Picha na Khamisi Miharo


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa