CRDB Marathon yachangia milioni 250,000,000 matibabu ya moyo kwa watoto
Picha na: Othman Michuzi na Khamis Mussa
********************************************************************************************
Na: Genofeva Matemu
Shilingi Milioni 250,000,000 zimetolewa na Benki ya CRDB
kupitia mbio za CRDB Marathon msimu wa tatu kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto
wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete.
Akikabidhi hundi ya fedha hizo leo katika viwanja vya Farasi
vilivyopo Oyster bay Jijini Dar es Salaam Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango alisema kuwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
ina uwezo wa kuwafanyia upasuaji mkubwa na mdogo wa moyo watoto 250 hadi 300
kwa mwaka ambayo ni sawa na asilimia 10 yamahitaji yote ya nchi kwa mwaka
Mhe. Dkt. Mpango alisema kuwa gharama za upasuaji wa moyo kwa
mtoto mmoja ni kati ya shilingi milioni mbili hadi milioni kumi na moja
ikitegemea na ukubwa wa tatizo hivyo kuishukuru Banki ya CRDB kuona umuhimu wa
kusaidia matibabu ya watoto wenye uhitaji wa kufanyiwa upasuaji wa moyo.
“Kwa takwimu zilizopo mpaka kufikia mwezi juni mwaka huu
Taasisi ya Moyo ina wagonjwa wa moyo takribani 750 ambao walihitaji kufanyiwa
upasuaji mkubwa na mdogo wa moyo kwa hiyo hii inadhihirisha ni kwa kiasi gani
fedha hizi mnazochangia kupitia CRDB Marathon zinaenda kupunguza changamoto ya
huduma ya matibabu katika jamii yetu”, alisema Mhe. Dkt. Mpango
“Nimefurahishwa kuona watanzania wengi pamoja na wananchi
kutoka nchi jirani wakijitokeza kuchangia watoto wetu ili waweze kupata huduma
ya upasuaji wa moyo kupitia ushiriki wenu kwenye mbio za CRDB Marathon,
nawaomba muendelee kuwa na moyo ya kujitoa kama huu kwa ajili ya kurejesha
tamasamu kwa wale ambao wanakutana na changamoto za kiafya” Mhe. Dkt. Mpango
Aidha Mhe. Dkt. Mpango alisema kuwa uamuzi wa CRDB Bank kutumia
marathon ya mwaka huu kuchangisha fedha kwa ajili ya akina mama wenye ujauzito
hatarishi ni sehemu ya kurejesha matumaini kwa akina mama ili waweze kupata
huduma stahiki katika hospitali ya CCBRT.
“Michango yenu itaokoa maisha ya akina mama na watoto wengi,
kwani mbio hizi zinatupa nafasi kama serikali kushirikiana na wadau kutafuta
suluhisho la changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa huduma za jamii”,
“Maendeleo ya nchi yanahitaji nguvu kazi yenye afya njema,
lakini watanzania wengi hasa sisi tunaoishi mijini tunakabiliwa na uzito
uliozidi na inasikitisha kuona vijana wengi wanapoteza maisha kutokana na
magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari na shinikizo la damu magonjwa ambayo
kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na mtindo wa maisha, ulaji usiofaa, na
kutokufanya mazoezi ya mara kwa mara”, alisema Mhe. Dkt. Mpango
Mhe. Dkt. Mpango alisema kuwa kupitia mbio za CRDB Marathon
CRDB wamekuwa sehemu ya kuelimisha watanzania juu ya kutunza afya kupitia mbio
hizo, kuweka utaratibu wa kufanya mazoezi kuwa wa kudumu kwa kila mmoja ili kujiepushe
na maradhi lakini pia kupunguza mzigo wa gharama za matibabu ya magonjwa
yanayoweza kuepukika kwa kufanya mazoezi mara kwa mara.
“Hata baada ya leo muendelee kuwahimiza watanzania kuishi
maisha yanayofuata misingi ya afya bora, kuendelea kufanya mazoezi, pamoja na
kuwa na bima za afya ili kurahishisha upatikanaji wa huduma za matibabu wakati
tunapofikwa na changamoto za kiafya”, alisema Mhe. Dkt. Mpango
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB
Abdulmajid Nsekela alisema kuwa moja ya malengo iliyojiwekea CRDB wakati
inandaa mbio hizo za msimu wa tatu ilikua ni pamoja na kufanikisha huduma za
matibabu ya moyo kwa watoto 125 kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni
250,000,000 jambo ambalo limefanikiwa kwa asilimia 100.
“Kipekee kabisa nawashukuru wote walioungana nasi katika mbio
za CRDB Marathon msimu wa tatu kwa ajili ya kufanikisha lengo hili, kujitokeza
kwenu kwa wingi kumeonesha dhamira ya kuwa watanzania tuna upendo wa dhati kwa
ndugu zetu hawa ambao wanahitiji huduma za matibabu”,
“Tunafahamu kwenye mbio hizi wamekuja washiriki zaidi ya
6,000 kutoka Tanzania pamoja na majirani zetu Kenya, huu ni upendo usiopimika
kuona hata majirani zetu wanashirikiana nasi kuchangia huduma za matibabu kwa
watoto na wanawake, tunawashukuru sana”, alisema Nsekela
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya bima ya maisha ya Sanlam Julius
Magabe alisema kuwa Sanlam imekuwa washirika wakuu katika mbio za CRDB Marathon
kwasababu sera yeo ya huduma za jamii inaamini katika kurudisha katika jamii
yenye uhitaji.
“Tunaipongeza CRDB Bank kwa kutuongoza katika taratibu hizi
za kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete, naipongeza pia taasisi hii kwa juhudi zao za kuokoa maisha ya watoto”,
alisema Magabe
Comments
Post a Comment