Wataalam wa afya jitokezeni kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi 2022: Mhe. Dkt. Alice Kaijage

Mbunge wa viti Maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage akielezea ujuzi atakaoupata katika mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwakutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yatakavyomsaidia katika taaluma yake wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Jijini Dar Es Salaam.


********************************************************************************************************************************

Wataalam wa afya nchini wameombwa kuiunga mkono Serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele kujitokeza na kuwaeleza wagonjwa wanaowahudumia umuhimu wa sense ya watu na makazi kwa maendeleo ya nchi.

Akizungumza wakati wa mafunzo ya jinsi ya kufanya kipimo cha kuangalia moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) leo Jijini Dar es Salaam Mbunge wa viti maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage alisema kuwa kwa maendeleo ya taifa lazima kuwe na takwimu hivyo ni vyema watu wakajitokeza kwa pamoja kuhesabiwa

“Kama madaktari inatupasa kujua idadi ya wagonjwa tunaowahudumia ili tuje kutoa takwimu sahahi ambazo zitaisaidia serikali kuweka miundombinu rafiki katika maeneo husika kulingana na idadi ya watu na kuwapa watanzania fursa ya kupata huduma za afya zilizo bora”,

“Sensa ya mwaka huu imedhamiria kuisaidia Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia katika maendeleo ya nchi pamoja na kuleta mageuzi katika sekta ya afya na jamii hivyo ni wakati wetu sasa kuhakikisha kuwa takwimu zinazopatikana wakati wa sensa ni sahihi hivyo kuboresha  sekta yetu afya”, alisema Mhe. Dkt. Alice

Akizungumzia zoezi la Sensa ya watu na makazi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema kuwa wataalam wa sekta ya afya ni muhimu kujua idadi ya watu kwasababu kuna baadhi ya magonjwa ambayo yanakwenda na rika kama yatapatiwa matibabu katika rika husika hivyo kuwaomba wananchi kuwa mstari wa mbele kutimiza adhma ya sense ya mwaka 2022 kwa maendeleo endelevu ya afya nchini

“Zoezi la Sensa litatusaidia sisi wataalam wa afya kupata takwimu halisi ya watanzania ili kuweka miundombinu ya afya itakayokidhi huduma za afya kwa watanzania wote”,

“Mfano hai, Tanzania kwa miaka mitano iliyopita kila mwaka wanazaliwa watoto milioni 2 ambapo kati ya hao asilimia 0.8 mpaka asilimia 1 ya watoto wanazaliwa na tatizo la moyo, na katika hiyo asilimia 1 asilimia 25 watahitaji upasuaji wa moyo, hivyo nisingekuwa na ile takwimu ya milioni 2 nisingeweza kupiga hizo hesabu, tutumie tarehe 23 Agosti kutimiza lengo la kupata takwimu ya watu na makazi nchini”, alismea Prof. Janabi

Sensa ya watu na makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka kumi, ambapo sense ya mwaka 2022 ni sense ya sita kufanyika nchini baada ya muungano wa Tanganika na Zanzibari mwaka 1964.

 


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)