CRDB Marathon yarudisha tabasamu kwa watoto 200 waliofanyiwa upasuaji wa moyo
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mbio za CRDB
Marathon msimu wa tatu zinazotarajiwa kufanyika tarehe 14 Agosti, 2022 kwa
ajili ya kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo pamoja na matibabu ya
wanawake wenye ujauzito hatarishi leo katika ukumbi wa mikutano wa Johari
Rotana uliopo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wadau mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakiendelea wakati wa mkutano na
waandishi wa habari kuhusu mbio za CRDB Marathon msimu wa tatu zinazotarajiwa
kufanyika tarehe 14 Agosti, 2022 kwaajili ya kuwasaidia watoto wenye magonjwa
ya moyo pamoja na matibabu ya wanawake wenye ujauzito
hatarishi leo katika ukumbi wa Johari Rotana uliopo jijini Dar es
Salaam.
Mkugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela akiungana na wakurugenzi wa
Taasisi washirika wa mbio za CRDB Marathon kutambulisha vifaa vitakavyotumika
katika mbio hizo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mbio hizo
msimu wa tatu zinazotarajiwa kufanyika tarehe 14 Agosti, 2022 kwaajili ya
kuwasaidia watoto wenye magonjwa ya moyo pamoja na matibabu ya wanawake
wenye ujauzito hatarishi leo katika ukumbi wa mikutano wa Johari Rotana
uliopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa
katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid
Nsekela pamoja na wadau kutoka taasisi mbalimbali wakati wa mkutano na
waandhishi wa habari kuhusu mbio za CRDB Marathon msimu wa tatu zinazotarajiwa
kufanyika tarehe 14 Agosti, 2022 kwaajili ya kusaidia watoto wenye magonjwa ya
moyo pamoja na matibabu ya wanawake wenye ujauzito
hatarishi leo katika ukumbi wa mikutano wa Johari Rotana uliopo jijini Dar
es Salaam.
***************************************************************************************
Na: Genofeva Matemu
Watoto
200 wenye magonjwa ya moyo wamefanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) kupitia fedha zilipatikana katika msimu wa kwanza na wa
pili wa CRDB Marathon.
Akizungumza
wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu msimu wa tatu wa mbio hizo
uliofanyika leo katika ukumbi wa Hoteli ya Johari Rotana iliyopo jijini Dar es
Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof.
Mohamed Janabi alisema kupitia mbio za CRDB watoto ambao familia zao hazina
uwezo wameweza kufanyiwa upasuaji wa moyo.
Prof.
Janabi alisema kwa misimu miwili ya mbio za CRDB wamewafanyia upasuaji wa moyo
watoto 200, ambapo kuna watoto kama wasingepata huduma za matibabu mapema labda
wengine wasingeweza hata kusherehekea mwaka mmoja wa kuzaliwa kwao.
“JKCI
ukiondoa Afrika ya Kusini sisi ndio tunafuata kuwa Taasisi ya kibingwa ya
magonjwa ya moyo, hivyo tunaushukuru uongozi wa CRDB na wadau wote wanaochangia
mbio hizi kwa lengo la kuokoa maisha ya watoto wenye uhitaji wa kupatiwa
matibabu ya moyo”, alisema Prof. Janabi
Prof.
Janabi aliwataka watanzania kujitokeza kushiriki mbio za CRDB kuendelea
kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo pamoja na wanawake
wajawazito wanaopitia changamoto mbalimbali zinazoweza kuwasababishia ugonjwa
wa fistula.
“Rai
yangu kwa watanzania nawaomba mjitokeze kushiriki mbio hizi za CRDB kuchangia
matibabu ya watoto na wanawake lakini pia niwakumbushe kuwa kila mtu ajisajili
kwenye mbio ambazo ana uwezo nazo kwani mazoezi yaliyopita kiwango ni hatari
kwa afya zetu”, alisema Prof. Janabi
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela
aliwashukuru wadau na wananchi ambao wamekuwa mstari wa mbele kujisajili na
kutoa michango mbalimbali kwaajili ya kuongeza tabasamu kwa watanzania wenye
uhitaji wa kupatiwa matibabu kupitia mbio hizo.
“Kama
ambavyo kauli mbiu ya mbio hizi inavyosema ‘Kasi isambazao tabasamu’ mbio hizi
zinalenga kumfurahisha kila mtu atakayeshiriki, kuleta uelewa wa changamoto
zilizopo katika jamii yetu, kuishirikisha jamii changamoto hizo pamoja na
kurejesha tumaini na kusambaza tabasamu kwa watoto wetu wenye uhitaji wa
upasuaji wa moyo JKCI na kuwagusa akina mama wenye ujauzito hatarishi
wanaotibiwa CCBRT”,.
“Msimu
wa tatu wa mbio za CRDB Marathon umelenga kukusanya fedha kwa ajili ya
kuendelea kuwafikia watoto wenye uhitaji wa kufanyiwa upasuaji wa moyo na
wanawake wenye ujauzito hatarishi ambapo hadi sasa watu zaidi ya 4,200 tayari
wameshajisajiri kushiriki mbio hizi na kati yao watu 801 ni wakimbiaji kutoka
nje ya nchi, haya ni mafanikio makubwa sana kwetu CRDB”,.
Nsekela
alisema benki hiyo iliona mafanikio makubwa yaliyopo katika Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kuwa hospitali kubwa ya kibingwa Afrika Mashariki na
Kati, yenye teknolojia ya hali ya juu, wataalam wabobezi na yenye vifaa vya
kisasa hivyo kupata motisha na kuona kuwa mahali sahihi kwa benki hiyo kuwekeza
katika matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo.
Naye
Mkurugenzi wa kampuni ya bima ya maisha ya Sanlam Julius Magabe alisema kampuni
hiyo inajivunia kuwa washirika wa mbio za CRDB kutokana na mbio hizo
kujikita zaidi katika kuhamasisha watu kusaidia jamii yenye uhitaji.
“Tunaishukuru
Benki ya CRDB kwa kuandaa mbio hizi zinazowaleta watanzania kushiriki katika
kutatua changamoto katika jamii, Sanlam ni kampuni ambayo inajali afya na
mazingira ya watu wake hivyo tunakila sababu ya sisi kushiriki katika mbio
hizi”, alisema Magabe.
Mbio
za CRDB zinatarajiwa kufanyika tarehe 14 Agosti 2022 ambapo mgeni rasmi atakuwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango, huku
viongozi mbalimbali wa Serikali wakimuunga mkono akiwemo Waziri wa Michezo Mhe.
Mohamed Mchengerwa, Naibu waziri wa Michezo Mhe. Pauline Gekule, Naibu Spika
Mhe. Mussa Zungu, Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa
Maji Mhe. Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa CCM Mhe. Daniel Chongolo na viongozi
kutoka Taasisi mbalimlbali nchini.
Comments
Post a Comment