Posts

Showing posts from 2023

WANANCHI 761 WAPATA HUDUMA YA TIBA MKOBA YA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumalizika kwa mbio za Siha Marathon 2023 zilizofanyika hivi karibuni mkoani Kilimanjaro. Wananchi wa Siha wakijadili mambo mbalimbali huku wakisubiri kufanyiwa vipimo vya moyo wakati wa kambi maalumu ya siku sita ya upimaji na matibabu ya moyo iliyomalizika hivi karibuni katika hospitali ya Wilaya ya Siha. Na: JKCI ********************************************************************************************** Watu 761 wamepata huduma ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya moyo katika kambi maalum ya matibabu iliyofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Wilaya Siha. Kambi hiyo ilifanyika kwa muda wa siku sita kuanzia tarehe 18 hadi 23/12/2023 ambapo watu w

Aliyebadilishwa valvu ya moyo aeleza hali ilivyokuwa

Image

Dkt. Mollel: Wataalamu wa Afya tengeni muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini

Image
 Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel na wataalamu wa Taasisisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na simba mweupe walipotembelea  shamba la wanyamapori  Serval Wildlife  kwaajili ya kufanya utalii wa ndani. Wataalamu wa JKCI walikuwa    katika Hospitali ya Wilaya ya Siha kwaajili ya kutoa    huduma za upimaji na matibabu ya moyo. Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya utalii wa ndani wa kuwalisha wanyama walati walipotembelea shamba la wanyamapori Serval Wildlife Siha llililopo wilayani Siha. Wataalamu wa JKCI walikuwa    katika Hospitali ya Wilaya ya Siha kwaajili ya kutoa    huduma za upimaji na matibabu ya moyo. Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na wacheza ngoma ya kimaasai wakati wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea shamba la wanyamapori  Serval Wildlife kwaajili ya kufanya utalii wa ndani. Wataalamu wa JKCI walikuwa katik

Balozi Polepole kushirikiana na JKCI kuboresha matibabu ya moyo

Image
Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuona namna ambavyo watashirikiana katika kuboresha huduma ya matibabu ya moyo. *********************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************    Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole amesema kuwa atashirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhakikisha watanzania wanaendelea kupata huduma bora za matibabu ya moyo. Mhe. Balozi Polepole ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kuona namna ambavyo nchi ya Cuba inaweza kushirikiana na Tanzania katika utoaji wa huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo. Alisema nchi ya Cub

Dkt. Mollel: Wananchi wengi zaidi kufikiwa na huduma za kibingwa za matibabu ya moyo

Image
Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel akimkabidhi   Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Dkt. Christopher Timbuka funguo za gari moja kati ya matatu yaliyotolewa na Serikali kwa wilaya hiyo ambalo litatumika katika huduma za afya. Licha ya kukabidhi gari hilo Mhe. Dkt. Mollel alifungua kambi maalumu ya matibabu ya moyo inayofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya wilaya ya Siha.  Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel akiukabidhi uongozi wa wilaya ya Siha vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 900 ambavyo vitatumika katika Hospitali ya wilaya ya Siha. Licha ya kukabidhi vifaa hivyo Mhe. Dkt. Mollel alifungua kambi maalumu ya matibabu ya moyo inayofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya wilaya ya Siha. Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa jimbo la Siha Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na

Siha wajitokeza kwa wingi kupima moyo

Image
Daktari bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophylly Ludovick akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Christopher Timbuka namna kipimo cha kuangali jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) kinavyofanyika wakati alipotembelea kambi    maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo inayofanyika katika Hospitali ya wilaya ya Siha. Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Christopher Timbuka akimsikiliza Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mainda Hamis wakati alipotembelea kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo inayofanyika katika Hospitali ya wilaya ya Siha. Daktari bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophylly Ludovick akiwafundisha wataalamu wa afya wa Hospitali ya Wilaya ya Siha namna ya kufanya kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo ya siku tano inayofanyika katika Hospitali hiyo. Pamoja na kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wanannchi   JKCI pi

Dkt. Timbuka awahimiza Siha kupima magonjwa ya moyo

Image
Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Christopher Timbuka akizungumza na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) pamoja na waratibu wa Siha Marathon waliofika ofisini kwake kwaajili ya kujitambulisha. Wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Wilaya ya Siha wanafanya kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo ya siku tano inayofanyika katika Hospitali ya wilaya ya Siha. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Dkt. Haji Mnasi akizungumza na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) pamoja na waratibu wa Siha Marathon waliofika ofisini kwake kwaajili ya kujitambulisha. Wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Wilaya ya Siha wanafanya kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo ya siku tano  katika  Hospitali ya wilaya ya Siha. Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akitoa elimu ya lishe bora kwa wananchi waliofika katika Hospitali ya wilaya ya Siha kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na mat

Upimaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wa wilaya ya Siha

Image

Uhakika wa upatikanaji wa dawa kwa wagonjwa wanaotibiwa JKCI

Image

Tanzania yavunja rekodi matibabu ya moyo

Image
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. John Jingu alimjulia hali Mchungaji Donald Lema ambaye amefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo wa kubadilisha valvu ya mshipa mkubwa wa damu (Aortic Valve) bila kufungua kifua (Transcatheter Aortic Valve Implantation procedure – TAVI) katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge. Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. John Jingu alimjulia hali Mzee Kutbuddin Fakhryddin Taibali  ambaye amefanyiwa  upasuaji mdogo wa moyo wa kubadilisha valvu ya mshipa mkubwa wa damu (Aortic Valve) bila kufungua kifua (Transcatheter Aortic Valve Implantation procedure – TAVI). Upasuaji huo umefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini katika kambi maalumu ya matibabu iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Starcare ya nchini India.  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. John Jingu akizungumza na wataalamu wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Hospitali ya Starcare ya nchi

Kwa mara ya kwanza Valvu ya moyo yabadilishwa bila kufanya upasuaji wa kufungua kifua

Image
Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Starcare ya nchini India wakifanya upasuaji mdogo wa moyo wa kubadilisha valvu ya mshipa mkubwa wa damu (Aortic Valve) bila kufungua kifua (Transcatheter Aortic Valve Implantation procedure – TAVI) katika kambi maalumu ya siku mbili ya matibabu ya moyo inayofanyika JKCI. Upasuaji huo mdogo wa kubadilisha valvu umefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini. Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Starcare ya nchini India wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kumfanyia mgonjwa upasuaji mdogo wa moyo wa kubadilisha valvu ya mshipa mkubwa wa damu (Aortic Valve) bila kufungua kifua (Transcatheter Aortic Valve Implantation procedure – TAVI) katika kambi maalumu ya siku mbili ya matibabu ya moyo inayofanyika JKCI. Upasuaji huo mdogo wa kubadilisha valvu umefanyika kwa mara ya kwanza hapa nch

Malawi wafurahia huduma za matibabu ya moyo

Image

SATF warudisha tabasamu la watoto wenye matatizo ya moyo

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea kutoka kwa Meneja wa Mradi wa Shirika la Social Action Fund (SATF) Nelson Rutabanzibwa mfano wa hundi ya shilingi milioni 60 fedha mbazo zimetolewa jana  kwaajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto 10. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimshukuru Meneja wa Mradi wa Shirika la Social Action Fund (SATF) Nelson Rutabanzibwa baada ya shirika hilo kutoa msaada wa shilingi milioni 60 fedha mbazo zimetolewa jana kwaajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto 10. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza jana mara baada ya kupokea msaada wa shilingi milioni 60 kutoka kwa Shirika la Social Action Fund (SATF) fedha mbazo zimetolewa kwaajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto 10. Meneja wa Mradi wa Shirika la Social Action Fund (SATF) Nelson Rutabanzibwa akizungumza jana

Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI wakutana jijini Dar es Salaam

Image
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina ambaye pia ni Mratibu wa huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto    Mkoa wa Rukwa akiongoza kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI    Dkt. Peter Kisenge. Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akiwaonesha mfano wa jengo litakalojengwa katika Hospitali ya JKCI Dar Group wajumbe wa bodi hiyo wakati wa kikao cha tano cha Bodi kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.  Baadhi ya Viongozi wa Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi     hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba katika mwaka wa fedha wa 2023/24 wakati wa kikao cha