Daktari bingwa wa Moyo kutoka Misri kufanya upasuaji JKCI

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimkaribisha Balozi wa Tanzania Nchini Misri Mhe. Emmanuel Nchimbi alipowasili katika Taasisi hiyo huku akiongozana na wageni kutoka Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) iliyopo nchini Misri kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tatizo Waane akielezea huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati ugeni kutoka Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) iliyopo nchini Misri ulipotembelea JKCI kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akizungumza na wageni kutoka Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) iliyopo nchini Misri kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni walipotembelea Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya viongozi wa menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wageni kutoka Taasisi ya Ushrikiano wa Afrika na Asia (AFASU) kutoka nchini Misri wakifuatilia taarifa iliyokua ikitolewa wakati wageni hao walipotembelea JKCI kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Tanzania Nchini Misri Mhe. Emmanuel Nchimbi akielezea umuhimu wa ujio wa wageni kutoka Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) kutoka nchini Misri walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) hivi karibuni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini.


Rais wa Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) kutoka nchini Misri Dkt. Hossam Darwish akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea JKCI kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Tanzania Nchini Misri Mhe. Emmanuel Nchimbi katika picha ya pamoja na viongozi wa menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wageni kutoka Taasisi ya Ushrikiano wa Afrika na Asia (AFASU) baada ya ziara yao JKCI kwa ajili ya kujenga mashirikiano katika masuala ya tiba ili kuboresha huduma za afya nchini hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Picha na: Khamis Mussa

**************************************************************************************

Nchi ya Misri kupitia Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Misri imefanikiwa kumleta daktari bingwa wa magonjwa ya moyo na upasuaji mdogo wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kubadilishana ujuzi na kujenga uwezo.

Akizungumza na vyombo vya habari hivi karibuni katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam Balozi wa Tanzania Nchini Misri Mhe. Emmanuel Nchimbi alisema kuwa katika mazingira ya ushirikiano baina ya Tanzania na Misri AFASU wameona ni muhimu kumleta Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo nia ikiwa ni kuendeleza mashirikiano ili kuboresha huduma za afya hapa nchini.

“Kama Ubalozi wa Tanzania nchini Misri tutaendelea kufanya jitihada ambazo zitaboresha zaidi eneo la afya ambapo kwa kuanzia leo tupo JKCI na daktari ambaye ni bingwa katika magonjwa ya moyo ili watanzania wenzetu wawe na afya bora kwa maendeleo ya nchi yetu”,

“Dkt. Ahmed Rezq ni daktari bingwa na mkufunzi wa vyuo vikuu vitatu duniani ambaye ameshafanya maelfu ya upasuaji wa moyo atakua katika Taasisi hii kwa muda wa siku nne akijitolea kuwahudumia wagonjwa wetu hapa nchini, naamini kwa siku hizi nne wataalam wetu watapata kitu kipya”, alisema Mhe. Nchimbi

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tiba ya Moyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tatizo Waane alisema kuwa JKCI imebahatika kupata ugeni kutoka nchini Misri ambao kwa pamoja wanaenda kuangalia ni kwa namna gani wataweza kujenga uwezo pamoja na kusaidia wagonjwa wanaotibiwa JKCI.

“Ujumbe huu umekuja JKCI kwa mara ya kwanza nia ikiwa ni kuongeza ushirikiano baina ya yetu na wao, kujenga uwezo wa Taasisi yetu katika kutibu magonjwa ya moyo na kuangalia ni kwa namna gani wanaweza kutusaidia sisi na nchi nyingine za Afrika katika kukabiliana na magonjwa ya moyo”,

“JKCI tangu kuanzishwa kwake mwaka 2015 imeshafanya upasuaji mdogo wa moyo kupitia tundu dogo kwenye paja kwa wagonjwa zaidi ya elfu 7, ambapo hadi sasa tuna aina za upasuaji zaidi ya 35 tunazofanya. Kupitia ugeni huu tutaweza kuongeza aina za upasuaji ambazo tunafanya tukiwa na lengo la kuwasaidia watanzania”, alisema Dkt. Waane

Naye Rais wa Taasisi ya Ushirikiano wa Afrika na Asia (AFASU)   kutoka nchini Misri Dkt. Hossam Darwish alisema kuwa wameona umuhimu wa kufanya kazi na JKCI kwasababu moja ya malengo yaliyopo katika Taasisi hiyo ni pamoja na kujali uhai wa binadamu.

“Namshukuru Mhe. Balozi Nchimbi kwa juhudi zake alizozifanya leo hii kutukutanisha nanyi, Taasisi yetu ya AFASU ilianza rasmi mwaka 1955 ikiwa na lengo la kuleta maendeleo ya binadamu, kumjali binadamu na kuakikisha anakua na afya njema”,

“Leo tupo hapa JKCI ili kushirikiane kwa pamoja, kushikana mikono kwa pamoja kuhakikisha uhai wa binadamu unaokolewa. Tumekuja na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka nchini Misri ambaye atakua nanyi hapa kwa kipindi cha siku nne kwa ajili ya kubadilishana uzoefu”, alisema 

 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa