Prof. Janabi: Matumizi makubwa ya chumvi ni hatari kwa afya ya moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya moyo duniani leo tarehe 29/09/2022. Katika kuadhimisha siku hiyo wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akitazama kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography) ambacho alipimwa mwananchi aliyefika Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya moyo. Katika kuadhimisha siku ya moyo duniani leo tarehe 29/09/2022 wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akitazama jinsi mwananchi anavyopimwa kipimo cha kuangalia shinikizo la damu (BP) wakati wa zoezi la siku tano la uchunguzi na matibabu ya moyo linalofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ikiwa ni maadhimisho ya siku ya moyo duniani tarehe 29/09/2022.
Wananchi wa mkoa wa Arusha waliofika Arusha Lutheran Medical Centre(ALMC) kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya moyo wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi awakati akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo na jinsi ya kuyaepuka katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo tarehe 29/09/2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wakazi wa Arusha kuhusu magonjwa ya moyo na jinsi ya kuyaepuka wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo tarehe 29/09/2022 katika viwanja vya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC).
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bridget Ndumbaro akiangalia mishipa ya damu ya mguu wa mwananchi aliyefika katika viwanja vya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo tarehe 29/09/2022.
Afisa muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Veronica Vedastus akimpima kipimo cha kuangali mfumo wa umeme wa moyo (Electrocardiography-ECG) mwananchi aliyefika katika viwanja vya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambako inafanyika kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo tarehe 29/09/2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea kuhusu umuhimu wa watoto wenye matatizo ya moyo kufanyiwa upasuaji mapema wakati wa kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC).
Mkurugenzi Mtendaji wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) Elisha Twisa akimkabidhi zawadi ya shukurani Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo tarehe 29/09/2022 katika viwanja vya ALMC. Katika kuadhimisha siku hiyo wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.
********************************************************************************************************************************************************************
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi amewataka wananchi hususani wa mkoa wa Arusha kuacha matumizi makubwa ya chumvi inayosababisha shinikizo la juu la damu ambalo moja ya madhara yake ni kutanuka kwa moyo.
Comments
Post a Comment