Watoto 77 wafanyiwa upasuaji wa moyo ndani ya wiki moja

Naibu Balozi wa Saud Arabia Nchini Tanzania Mhe. Abdallah Al - Harbi akiwapongeza madaktari kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia kwa ushirikiano wanaoufanya katika kutoa huduma za matibabu ya moyo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyomalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Asha Mahita akielezea umuhimu wa ushirikiano katika kutoa huduma za afya hapa nchini wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) kutoka nchini Saudi Arabia Loay Abdulsamad akieezea matibabu waliyoyatoa kwa watoto wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Idara ya Mashiriki ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Hemedi Mgaza akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa upasuaji mkubwa wa moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau akiwashukuru madaktari kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia kwa kuendelea kushirikiana na madaktari wa JKCI wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari hao na kumalizika leo katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wataalam wa afya wakifuatili yaliyokuwa yakiendelea wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wataalam wa afya wakifuatili yaliyokuwa yakiendelea wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Mama wa Mtoto aliyefanyiwa Upasuaji mkubwa wa moyo kutoka Mkoani Kigoma Hadija Yusufu akitoa neno la shukrani kwa madaktari waliomfanyia upasuaji mtoto wake wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyofanywa na madakari wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia na kumalizika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Naibu Balozi wa Saud Arabia Nchini Tanzania Mhe. Abdallah Al – Harbi katika picha ya pamoja na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia baada ya mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. 

Picha na: Khamis Mussa

 

**************************************************************************************************

Watoto 77 wamefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo iliyofanywa na madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia

Katika kambi hiyo watoto 47 wamefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo kupitia tundu dogo kwenye paja kwa kutumia mtambo wa Cathlab na watoto wengine 30 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua kifua.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema kuwa watoto waliofanyiwa upasuaji katika kambi hiyo waliokuwa na matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo ambayo ni matundu na mishipa ya damu ya moyo kutokuwa katika mpangilio maalum.

“Wagonjwa 77 kwa muda wa wiki moja kufanyiwa upasuaji sio kitu kidogo, Taasisi nyingi zinazofanya upasuaji wa moyo inaweza kuwachukua mwaka mmoja kumaliza watoto 77, nawapongeza wataalam hawa kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya kwa wiki moja”,

“Wataalam kutoka nchini Saudi Arabia wamekuja na vifaa vya kisasa ambavyo huwa tunavitumia na gharama zake huwa ni kubwa lakini kupitia kambi hii tumeweza kuwafanyia upasuaji watoto ambao wanatoka kwenye familia zisizokuwa na uwezo hivyo kuwafanyia upasuaji wa moyo bila gharama”, alisema Prof. Janabi

Prof. Janabi alisema kuwa upasuji uliofanyika ulikua wa mafanikio na wa hali ya juu kwani baadhi ya watoto walikua na uzito mdogo kama kilo nne hivyo kufanya matibabu hayo kutokuwa rahisi lakini kupita wataalam hao watoto wote 77 wamefanyiwa upasuaji bila kupoteza mtoto hata mmoja.

“kipitia kambi hii maalum ya matibabu ya moyo watoto wamepata nafasi ya kuendelea kuishi maisha ambayo hayatakuwa na changamoto za magonjwa ya moyo kwani upasuaji waliofanyiwa unafanyika mara moja na mtoto anapona kabisa”,

“Kwa niaba ya wataalam wenzangu nawashukuru sana Wizara ya Afya, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha wataalam hawa kuendelea kuja na kutoa huduma ya matibabu kwa watoto wenye magonjwa ya moyo wanaohitaji upasuji”, alisema Prof Janabi

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Asha Mahita amewapongeza madaktari kutoka nchini Saudi Arabia kwa kuendelea kutoa msaada wa matibabu kwa watoto wenye uhitaji wa matibabu ya moyo na ujuzi wanaoutoa kwa wataalam wa afya hapa nchini hivyo kuboresha huduma za afya hasa huduma ya upasuaji wa moyo kwa watoto.

“Kwetu sisi Wizara haya ni mafanikio makubwa sana yamefanyika kwa kipindi kifupi kuokoa maisha ya watoto wetu, Kambi maalum za matibabu zina manufaa sana kwani hutusaidia kupata ujuzi zaidi na kujenga mahusiano baina ya nchi yetu na nchi ambazo wamekua nasi katika kubadilishana ujuzi wa kitabibu”, alisema Dkt. Asha

Akizungumza wakati wa mkutano huo Daktari wa wagonjwa waliolazwa katika Chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) Loay Abdulsamad alisema kuwa wataalam kutoka Saudi Arabia wamekua na uhusiano na JKCI kwa kipindi cha miaka saba uhusiano ambao umeleta mafanikio makubwa na kuongeza ujuzi kwa wataalam hao.

“Tunafanya kambi za matibabu ya moyo katika nchi mbalimbali lakini tunajisikia furaha kufanya kambi hizi hapa Tanzania kutokana na ukarimu wa watu wake lakini pia wataalam wa hapa ujuzi wao umekua ukiongezeka kwa kasi tofauti na tulivyoanza uhusiano huu wa kubadilishana ujuzi katika kutoa tiba mwaka 2015”,

“Tutaendelea na kambi za matibabu ya moyo kwa watoto hapa JKCI tukiwa na lengo la kuwasaidia watoto ambao wanatoka katika familia zisizokuwa na uwezo wa kumudu gharama za matibabu ili watoto hao nao waweze kupata nafasi nyingine ya kuishi bila ya kusumbuliwa na maradhi ya moyo”, alisema Dkt. Abdulsamad

Akitoa neno la Shukrani Mzazi ambaye mtoto wake amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi hiyo Hadija Yusuph mkazi wa Kigoma amewashukuru wataalam hao kwa kuokoa maisha ya mtoto wake baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila ya kujua tatizo alilonalo mwanaye hadi alipofika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa ajili ya matibabu.

“Nawashukuru sana madaktari ambao wamepambania maisha ya mtoto wangu ambaye hapo awali hatukujua anasumbuliwa na nini hadi tulipofika JKCI, sasa naona mabadiliko baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo nawashukuru sana”, alisema Hadija


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa