Dkt.Mwinyi aongoza matembezi ya kuhamasisha upimaji wa moyo na kufanya mazoezi
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akishiriki katika Matembezi ya Kuhamasisha Ufanyaji wa Mazoezi “Tembea na JKCI
Linda Afya ya Moyo Wako” na Kufunga Kambi ya Upimaji wa Moyo iliyofanyika
katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Unguja kuazia 23-27, Januari 2023,
matembezi hayo yaliyoanzia katika viwanja vya Maisara Suleiman na kumalizikia
katika Uwanja wa Amaan Unguja leo 28-1-2023 (kushoto kwa Rais) ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.Peter Kisenge, Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Naibu Waziri wa Afya
Zanzibar Mhe. Hassan K.Hafidh na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu
Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said na (kulia kwa Rais) Waziri wa Afya Zanzibar
Mhe. Nassor Ahmed Mazrui na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrissa
Mustafa Kitwana.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Hussein Ali Mwinyi, akishiriki katika mazoezi ya viungo yakiongozwa na Kocha Mkuu wa Mazoezi ya Viungo Zoni D. Ndg. Ahmad Rajab, baada ya kumalizika kwa Matembezi ya Kuhamasisha Upimaji wa Moyo na kufanya mazoezi “Tembea na JKCI Linda Afya ya Moyo Wako” yaliyoanzia katika viwanja vya Maisara Suleiman na kumalizikia katika Uwanja wa Amaan Unguja na(kulia kwa Rais) ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui na (kushoto kwa Rais) Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.Peter Kisenge.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishiriki katika mazoezi ya viungo baada ya kumalizika kwa Matembezi ya Kuhamasisha Upimaji wa Moyo na kufanya mazoezi “Tembea na JKCI Linda Afya ya Moyo Wako” yaliyoanzia katika viwanja vya Maisara Suleiman na kumalizikia katika Uwanja wa Amaan Unguja. Matembezi hayo yaliongozwa na RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Hussein Ali Mwinyi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia baada ya kumalizika kwa
Matembezi ya Kuhamasisha Upimaji wa Moyo na ufanyaji wa Mazoezi “Tembea na JKCI
Linda Afya ya Moyo Wako” na kufunga Kambi ya Upimaji wa Moyo, iliyofanyika
katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Unguja Jijini Zanzibar 23-27,Januri 2023,
matembezi hayo yalimalizika katika Uwanja wa Amaan Unguja.
MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza baada ya kumalizika kwa Matembembezi ya Kuhamasisha Upimaji wa Moyo na kufanya mazoezi “Tembea na JKCI Linda Afya ya Moyo Wako” na ufungaji wa Kambi ya Upimaji wa Moyo iliyofanyika katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja iliyoaza 23-27,Januari 2023, ufungaji huo uliyofanyika katika uwanja wa Amaan Unguja Jijini Zanzibar.
WAZIRI wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Hussein Ali Mwinyi, kuzungumza na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Matembezi ya Kuhamasisha Upimaji wa Moyo na kufanya mazoezi “Tembea na JKCI Linda Afya ya Moyo Wako” na ufungaji wa Kambi ya Upimaji wa Moyo iliyofanyika katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Unguja Jijini Zanzibar, iliyoaza 23-27,Januari 2023, matembezi hayo yaliyomalizikia katika uwanja wa Amaan Unguja.
**********************************************************************************************************************************************************************************
RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewataka
wananchi kubadili mfumo wa maisha kwa kufanya mazoezi ili kujikinga na magonjwa
mbalimbali yasioambukiza ukiwemo ugonjwa wa moyo.
Alisema hatua
hiyo imethibitishwa na wataalamu
wa afya kupitia utafiti walioufanya unaoonesha moja ya hatua muhimu ya
kukabiliana na magonjwa hayo ni kufanya mazoezi.
“Nawasihi nyote muendelee kushiriki kwenye kambi
mbalimbali za upimaji wa magonjwa na matembezi kama haya, kwani ni muhimu kwa
afya zenu, kila mtu huko anakoishi atambue kufanya mazoezi ni kinga muhimu
katika kuepuka magonjwa mengi hasa yasio ambukiza, kwa hiyo sote tuhimizane tujenge
utamaduni wa kufanya mazoezi na kupima afya zetu mara kwa mara ili kubaini
mapema kama tuna matatizo ya kiafya, kuchukue hatua za matibabu” Alishauri Dk.
Mwinyi.
Rais Dk. Mwinyi
aliyasema hayo viwanja vya Amani, Zanzibar alipofunga kambi ya upimaji na matibabu
ya moyo na kampeni ya kufanya mazoezi yenye kauli mbiu “Tembea JKCI, Linda Afya ya Moyo Wako”.
Alisema taifa
linatumia pesa nyingi za kigeni kugharamia
matibabu ya moyo na magonjwa mengine nje ya nchi. Hivyo aliipongeza taasisi ya
JKCI kwa kubunifu mikakati mbali mbali ya kinga na tiba ya maradhi ya moyo
nchini.
Aidha, aliishukuru taasisi hiyo kwa kuwajengea uwezo
watumishi wa afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuwasihi kuendeleza
utamaduni huko kwa watumishi wa Pemba.
“Nawasihi JKCI mfike na Pemba kwa ajili ya uchunguzi
na kuhamasisha ufanyaji wa mazoezi kama njia bora ya kuimarisha afya, bila ya
shaka wananchi wa Pemba nao wanahitaji huduma zenu na elimu hii kama
mlivyofanya hapa Unguja” Alishauri Dk. Mwinyi.
Katika hatua
nyengine Rais Dk. Mwinyi aliitaka
taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete kuongeza huduma zao kwenye maeneo mbalimbali ya nchi na kueleza
kuwa kuwepo kwao kutasaidia kupambana na matatizo mbali mbali ya afya ambayo
jamii wanakabiliana nayo.
Alieleza hatua hiyo itasaidia kuongeza uwezo na
wataalamu watakao wahudumia vizuri wananchi na kupunguza madhara ya magonjwa
haya ambayo yanaongezeka kila siku.
Alisema tokea kuanzishwa kwa taasisi hiyo, mwaka 2015 tayari
imesaidia wagonjwa wengi wakiwemo waliotibiwa kwa dawa na waliofanyiwa upasuaji
na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa, hivyo aliitaka taasisi hiyo kuimarisha
utendaji wao na kuongeza tija kwa watu wengi kunufaika na huduma zao.
“Nafahamu kuwa taasisi hii imekuwa na utendaji mzuri
sana tokea ilipoanzishwa. Hata hivyo, bado kuna nafasi ya kufanya vizuri zaidi
ili kuyafikia malengo ambayo Tanzania tumejiwekea, katika kuimarisha afya za
wananchi kwa kutoa huduma bora na zenye kiwango cha kimataifa”. Alieleza.
Akizungumza kwenya hafla hiyo, Waziri wa Afya, Nassor
Mazurui alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar watashirikiana na taasisi ya JKCI,
kuongeza wataalam wa matatizo ya moyo Zanzibar kutokana na uhaba wa wataalamu
hao ambapo alieleza kwasasa wapo wawili tuu.
Alisema alisema Zanzibar kwa sasa ina madaktari bingwa
wawili tuu wanaoshughulikia matatizo ya moyo.
Naye,
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter
Richard Kisenge, alisema taasisi yao kwa kushirikiana na Wizara ya Afya
Zanzibar, kupitia hospitali kuu ya Mnazi Mmoja wataendeleza matibabu ya moyo
kwa kutoa huduma za uzibuaji wa mishipa ya damu ya moyo na upasuaji mkubwa wa moyo
kwa wananchi ili kudumisha ushirikiano wao kwa vitendo.
Alisema
kampeni walioifanya wiki nzima Unguja alieleza walifanikiwa kuwahudumia
wagonjwa 718, wakubwa 627 na watoto 91 ambao walifanyiwa vipimo vya matibabu ya
moyo, sukari na magonjwa mengine.
Dk.
Kisenge aliongeza kati ya watu wazima 627 waliopimwa matatizo ya moyo, 549 waligunduliwa
wana ugonjwa wa moyo alieleza katika hatua hiyo walitoa rufaa 75 kwa baadhi ya
wagonjwa na kueleza kuwa 46 walipewa watu wazima na rufaa 29 walipewa watoto.
Kampeni
ya upimaji magonjwa yasiyoambukiza ya (JKCI)na ufanyaji wa mazoezi iliadhimishwa kwa kauli mbiu yao “TEMBEA NA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) na
WIZARA YA AFYA, LINDA AFYA YA MOYO WAKO”.
IMETAYARISHWA
NA IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.
Comments
Post a Comment