JKCI kukisimamia na kukijengea uwezo kitengo cha Moyo cha Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH)
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) Dkt. Brian Mawala jinsi Taasisi hiyo ilivyojipanga kuhakikisha hospitali hiyo inatoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.Wizara ya Afya imeipa JKCI kitengo cha Moyo kilichopo katika Hospitali hiyo ili ikisimamie na kukijengea uwezo katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo katika kanda ya Ziwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi hiyo pamoja na wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) mara baada ya kumalizika kwa kikao ambacho kilijadili namna ambavyo JKCI itakisimamia kitengo cha Moyo kilichopo katika Hospitali hiyo ili kiweze kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo katika kanda ya Ziwa.
Comments
Post a Comment