Wauguzi wa JKCI watoa huduma za upimaji na elimu ya magonjwa ya moyo mkoani Dodoma
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Adam Ndamayape akimweleza mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo
kuhusu ugonjwa wa shinikizo la juu la damu wakati
wa maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga yanayoenda sambamba na maonesho ya siku
tatu ya huduma zinazotolewa na wauguzi yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere
Square jijini Dodoma.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rehema Bakari akimpima mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo shinikizo la damu wakati wa maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga yanayoenda sambamba na maonesho ya siku tatu ya huduma zinazotolewa na wauguzi yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Wananchi waliofika katika Banda la Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakipata huduma za upimaji na elimu ya magonjwa ya
moyo wakati wa maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga yanayoenda sambamba na maonesho ya
huduma zinazotolewa na wauguzi yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere Square
jijini Dodoma.
Comments
Post a Comment