Mhe. Mazrui aipongeza JKCI kwa kutoa huduma Maonesho ya Afya Zanzibar


Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui akimsikiliza Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Eva Wakuganda alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya wiki ya Afya Zanzibar yanayoendelea katika viwanja vya Hoteli ya Golden Tulip Airport.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika lisilo la kiserikali Heart Team Africa Foundation (HTAF) Linda Gideon akimkabidhi kadi ya kuchangia matibabu ya moyo kwa watoto mwananchi wa Zanzibar mara baada ya kutoa mchango wake wakati wa maonesho ya wiki ya Afya Zanzibar yanayoendelea katika viwanja vya Hoteli ya Golden Tulip Airport.


Baadhi ya Wananchi wa Zanzibar wakiendelea kupata huduma katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya wiki ya Afya Zanzibar yanayoendelea katika viwanja vya Hoteli ya Golden Tulip Airport.

Na: JKCI

******************************************************************************************************************

Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui ameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushiriki maonesho ya wiki ya afya Zanzibar na kutoa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo pamoja na kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa hayo kwa wakazi wa Zanzibar.

Pongezi hizo zimetolea na Waziri huyo alipotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya Wiki ya Afya Zanzibar yanayofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport.

“Nawapongeza JKCI kwa kuwafikishia wakazi wa Zanzibar elimu na huduma hizi muhimu za matibabu ya moyo, mmekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa na huduma hizi” alisema Mhe. Mazrui

Mhe. Mazrui ameitaka JKCI kuendelea kuwahudumia wakazi wa Zanzibar bila kuchoka kwani wakazi hao wanawahitaji.

Aidha Mhe. Mazrui ameipongeza Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kutumia maonesho hayo kutafuta fedha za kusaidia upasuaji wa moyo kwa watoto wanaotibiwa JKCI.


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa