Wananchi wahimizwa kutumia kampeni ya “Jua Namba Zako” kupima afya zao SABASABA
Daktari wa wagonjwa wa dharura wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospital ya Dar Group Peace Masaoe akimuelezea huduma za dharura zinazotolewa na Taasisi hiyo Mwenyekiti Tume ya Madini Dkt. Janeth Lekashingo alipotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Juliaus Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Daktari bingwa wa
upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thabiti Ramadhani
akimpatia zawadi Kamishna wa Tume ya madini Mhandishi Thenestina Mwasha alipotembelea
banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar
es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Juliaus Kambarage
Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yapongezwa kufikisha kampeni
ya Jua Namba Zako katika maonesho ya SABASABA kuiamasisha jamii kufanya
uchunguzi wa viashiria vya magonjwa ya moyo kupitia maonesho hayo.
Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Madini Dkt.
Janeth Reuben alipotembelea banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya
50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika
katika Viwanja vya Mwalimu Juliaus Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya
Kilwa jijini Dar es Salaam.
Dkt. Janeth alisema kampeni hiyo inatoa fursa kwa wananchi
kutambua hali zao za afya mapema na kuchukua hatua za mapema dhidi ya magonjwa
ya moyo na magonjwa mengine yasiyoambukiza.
“Nimefika katika banda la JKCI na nimejione kwa macho namna
ambavyo huduma zinatolewa hapa, uwepo wa kampeni ya Jua Namba Zako katika
maonesho haya ni fursa muhimu kwa jamii kupima na kutambua afya zao hivyo
watumie vizuri maonesho haya kupima na kutambua namba zao”, alisema Dkt. Janeth.
Dkt. Janeth alisema sambamba na kampeni hiyo JKCI inatoa
elimu kuhusu magonjwa ya moyo pamoja na kuwafanyia wananchi vipimo vikubwa vya
moyo kwa urahisi bila hata kuvifuata hospitalini.
Aidha Dkt. Janeth amewaomba wananchi wanaotembelea maonesho
hayo wasisite kufika katika banda la JKCI na kuchangia matibabu ya watoto wenye
magonjwa ya moyo wanaotibiwa na Taasisi hiyo kupitia Taasisi isiyo ya
Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) inayofanya jukumu hilo la
kutafuta fedha za matibabu ya watoto.
Comments
Post a Comment