Naibu Katibu Mkuu Afya atembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya leo katika Taasisi hiyo iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akielezea namna ambavyo wagonjwa wa nje wanavyohudumiwa wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna  huduma za matibabu zinavyotolewa kwa wogonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akitoa  taarifa za watumishi wa Taasisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia taarifa mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa ziara fupi ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

 




 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari