Naibu Katibu Mkuu Afya atembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif
Shekalaghe akizungumza na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya leo katika Taasisi hiyo iliyopo Upanga
jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu akielezea namna ambavyo wagonjwa wa nje wanavyohudumiwa wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna huduma za matibabu zinavyotolewa kwa wogonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akitoa taarifa za watumishi wa Taasisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment