Posts

Showing posts from February, 2023

Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI watembelea Hospitali ya JKCI Dar Group

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya dharura wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Shamira Rwegoshora akiwaelezea wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo huduma za matibabu zinazotolewa kwa wagonjwa wa dharura wakati wajumbe hao walipotembelea leo JKCI Dar Group iliyopo eneo la TAZARA jijini Dar es Salaam. Mtaalamu wa tibaviungo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Jacqueline Mariki akifafanua jambo wakati wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Hospitali hiyo  leo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Mkuu wa Idara ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Rose Elibariki akiwaeleza huduma zinazotolewa katika wodi ya wazazi wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wajumbe hao walipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu akijadiliana n

Wajumbe wa Bodi ya Udhamini ya JKCI wapewa mafunzo ya kuwajengea uwezo zaidi wa kusimamia uendeshaji wa huduma

Image
Mwezeshaji kutoka Taasisi ya Uongozi Dkt. Lufunyo Hussein akiwafundisha wajumbe wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kusimamia utekelezaji wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo leo katika Ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. JKCI imeandaa mafunzo ya siku mbili ya  kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya Taasisi hiyo ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji wa bodi kwa ufanisi mkubwa. Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afya na Sayansi Shirikishi Bugando (CUHAS) Prof. William Mahalu akielezea namna ambavyo bodi hiyo inavyosimamia kazi zinazofanywa na Taasisi hiyo wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo zaidi wajumbe hao wa bodi ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji kwa ufanisi zaidi.   Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugen

HAKUNA MGONJWA ALIYEKUFA KWA KUKOSA PACEMAKER

Image
Madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Tulizo Shemu na Yona Gandye wakimwekea mgonjwa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri  (Pacemaker) leo tarehe 24/02/2023  ********************************************************************************************************************** Dar es Salaam, 24/02/2022 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI   HAKUNA MGONJWA ALIYEKUFA KWA KUTOKUWEKEWA “PACEMAKER”   Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kutoa ufafanuzi wa Habari iliyosambaa katika mitandaoni ya kijamii kuwa “Huduma ya Pace Maker haipo Muhimbili, Wagonjwa wanakufa” taarifa hiyo siyo ya kweli na ipuuzwe, kwani hakuna mgonjwa aliyekufa kutokana na tatizo la kutokuwekewa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri “Pacemaker”. Taasisi ilikuwa na upungufu wa Pacemaker kwa muda wa wiki mbili ilitokana na mtoa huduma ya kusambaza vifaa hivyo kuchelewa kuvileta hapa nchini kutoka nchini Uholanzi. Hata hivyo, iwapo inatokea upungufu wa vifaa hivi T

Shambulio la moyo hutokea ghafla, chukueni hatua kukabiliana nalo

Image

Wataalamu wa afya 300 washiriki kongamano la shambulio la moyo

Image
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shakalaghe akimpa cheti cha kutambua umuhimu wake katika kutoa huduma za matibabu ya moyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu wakati wa kufunga mkutano wa kwanza wa shambulio la moyo uliofanyika katika Hoteli ya Ledger Plaza jijini Dar es Salaam. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shakalaghe akimpa cheti cha kutambua umuhimu wake katika kutoa huduma za matibabu ya moyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa kufunga mkutano wa kwanza wa shambulio la moyo uliofanyika katika Hoteli ya Ledger Plaza jijini Dar es Salaam. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shakalaghe akimsikiliza Afisa Mauzo kutoka kampuni ya usambazaji wa dawa ya SUN PHARMA Innocent Maro lipotembelea kuona huduma zinazotolewa na kampuni hiyo wakati wa kufunga mkutano wa kwanza wa shambulio la moyo uliofanyika katika Hoteli ya Ledger Plaza jijini Dar es Salaam

Kuchunguza afya kusisubiri kuwa na dalili za kuumwa, shambulio la moyo h...

Image

Wataalam wa afya wakutana kujadili mbinu za kukabiliana na tatizo la sha...

Image

Dkt. Mollel atoa wito kwa wananchi kujitokeza kupima magonjwa ya moyo

Image
Naibu Waziri wa Afya Mhe.Dkt.Godwin Mollel akitoa tuzo kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof. Laurance Museru   ya kutambua mchango wake wa kuanzishwa kwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mkutano wa kwanza wa shambulio la moyo uliofanyika katika Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach, jijini Dar es Salaam. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Dkt. Maneno Mlawa akipokea tuzo kwa niaba ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Mhe.Dkt.Godwin Mollel ya kutambua mchango wake wa kuanzishwa kwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mkutano wa kwanza wa shambulio la moyo uliofanyika katika Hoteli ya  Ledger Plaza,  Beach jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI Prof. William Mahalu. Naibu Waziri wa Afya Mhe.Dkt.Godwin Mollel akitoa tuzo kwa Daktari bingwa wa moyo kutoka Chennai India Ulhas Pandurangi kwa ajili ya kumshukuru kwa kufundisha mfumo wa umeme wa moyo katika mkut

Kongamano la kwanza la shambulio la moyo kufanyika nchini

Image
Mkurugenzi Mtendaji   wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  Dkt. Peter Kisenge akizungumza na Waandishi wa Habari hawapo pichani kuhusu Mkutano wa shambulio la moyo unaotarajiwa kufanyika tarehe 17-18  mwezi huu katika hoteli ya Bahari Beach Jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Khuzeima Khanbhai akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanzishwa kwa kliniki ya maumivu ya kifua yenye lengo la kuhakikisha wagonjwa wa shambulio la moyo wanapata matibabu kwa wakati. Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Pedro Pallangyo akiwaeleza waandishi wa habari umuhimu wa kufuata mtindo bora wa maisha ili mtu aweze kujiepusha na magonjwa yasiyo ya kuambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo.       Mkurugenzi wa matibabu ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumzia na Waandishi wa Habari  kuhusu wagonjwa wa shambulio la moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. *****

JKCI yapata kibali kufundisha madaktari wa moyo kupitia COSECSA

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea cheti cha kuipa kibali JKCI kuwa Chuo cha kufundisha madaktari wa upasuaji wa moyo kupitia Chuo cha Madaktari wa upasuaji Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (COSECSA) kutoka kwa Mhadhiri wa Chuo cha COSECSA Dkt. Kitugi Nungu jana Jijini Dar es Salaam Daktari bingwa wa upasuaji mkubwa wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Bashiri Nyangasa akipokea cheti cha kumpa kibali kuwa mkufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi hiyo kutoka kwa Mhadhiri wa Chuo cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na kusini mwa Afrika (COSECSA) Dkt. Kitugi Nungu jana Jijini Dar es Salaam  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi cheti cha kumpa kibali kuwa mkufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi hiyo Daktari bingwa wa Upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Evarist Nyawawa kilichotolewa na Chuo cha Madakta

Wataalamu wa JKCI Waadhimisha siku ya wapendanao kwa kufanya upasuaji wa moyo kwa watoto 28

Image
Wataalam wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya upasuaji wa kuziba tundu la moyo katika kambi maalum ya matibabu ya siku tano inayofanywa na wataalamu wazawa wa Taasisi hiyo ambapo watoto 28 walifanyiwa upasuaji. Wataalam wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya upasuaji wa kuzibua mshipa wa damu wa moyo uliokuwa umeziba wakati wa kambi maalum ya siku tano iliyofanywa na madaktari hao ambapo watoto 28 walifanyiwa upasuaji. Na: JKCI ********************************************************************************************************* Watoto 28 wenye magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi maalumu ya siku tano ya matibabu ya moyo inayofanywa na madaktari wazawa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kambi hiyo maalum ya upasuaji wa moyo ilifanyika kwa lengo la kusherehekea siku ya wapendanao itakayofanyika duniani kote