Wajumbe wa Bodi ya Udhamini ya JKCI wapewa mafunzo ya kuwajengea uwezo zaidi wa kusimamia uendeshaji wa huduma


Mwezeshaji kutoka Taasisi ya Uongozi Dkt. Lufunyo Hussein akiwafundisha wajumbe wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kusimamia utekelezaji wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo leo katika Ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. JKCI imeandaa mafunzo ya siku mbili ya  kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya Taasisi hiyo ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji wa bodi kwa ufanisi mkubwa.


Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afya na Sayansi Shirikishi Bugando (CUHAS) Prof. William Mahalu akielezea namna ambavyo bodi hiyo inavyosimamia kazi zinazofanywa na Taasisi hiyo wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo zaidi wajumbe hao wa bodi ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji kwa ufanisi zaidi. 

Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili yanayotolewa jijini Dar es Salaam na Taasisi ya Uongozi kwa wajumbe wa bodi ya wadhamini ya Taasisi hiyo.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mratibu wa huduma za Afya ya uzazi na mtoto Mkoa wa Rukwa Asha Izina akielezea namna ambavyo bodi hiyo imejipanga kuboresha huduma zinazotolewa na JKCI wakati wa mafunzo ya siku mbili yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. JKCI imeandaa mafunzo hayo ya siku mbili ya  kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya Taasisi hiyo ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji wa bodi kwa ufanisi zaidi.

Mjumbe wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adv. Haruni Matagane ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa Serikali akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya JKCI ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji kwa ufanisi zaidi yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi jijini Dar es Salaam.


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Andrea Pembe akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya JKCI ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji kwa ufanisi zaidi yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA.Godfrey Kilenga ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ukaguzi wa mahesabu ,TAB Consult akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa bodi ya JKCI ili waweze kufanya kazi zao za uendeshaji kwa ufanisi zaidi yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari