JKCI yapata kibali kufundisha madaktari wa moyo kupitia COSECSA


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea cheti cha kuipa kibali JKCI kuwa Chuo cha kufundisha madaktari wa upasuaji wa moyo kupitia Chuo cha Madaktari wa upasuaji Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (COSECSA) kutoka kwa Mhadhiri wa Chuo cha COSECSA Dkt. Kitugi Nungu jana Jijini Dar es Salaam


Daktari bingwa wa upasuaji mkubwa wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Bashiri Nyangasa akipokea cheti cha kumpa kibali kuwa mkufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi hiyo kutoka kwa Mhadhiri wa Chuo cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na kusini mwa Afrika (COSECSA) Dkt. Kitugi Nungu jana Jijini Dar es Salaam 

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi cheti cha kumpa kibali kuwa mkufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi hiyo Daktari bingwa wa Upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Evarist Nyawawa kilichotolewa na Chuo cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na kusini mwa Afrika (COSECSA) jana Jijini Dar es Salaam

Mhadhiri wa Chuo cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na kusini mwa Afrika (COSECSA) Dkt. Kitugi Nungu akimkabidhi cheti cha kumpa kibali kuwa mkufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Alex Joseph wakati uongozi kutoka chuo hicho ulipowasilisha vyeti hivyo kwa wakufunzi wa JKCI jana jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi kutoka Chuo cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Africa (COSECSA) na madaktari wa JKCI waliotambuliwa na chuo hicho kuwa wakufunzi wa kozi ya upasuaji wa moyo katika Taasisi hiyo mara baada ya kukabidhiwa vyeti jana jijini Dar es Salaam


Picha na: JKCI

*****************************************************************************************************************


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari