Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya JKCI watembelea Hospitali ya JKCI Dar Group

Daktari bingwa wa magonjwa ya dharura wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Shamira Rwegoshora akiwaelezea wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo huduma za matibabu zinazotolewa kwa wagonjwa wa dharura wakati wajumbe hao walipotembelea leo JKCI Dar Group iliyopo eneo la TAZARA jijini Dar es Salaam.

Mtaalamu wa tibaviungo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Jacqueline Mariki akifafanua jambo wakati wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Hospitali hiyo  leo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.


Mkuu wa Idara ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Rose Elibariki akiwaeleza huduma zinazotolewa katika wodi ya wazazi wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wajumbe hao walipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma zinazotolewa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu akijadiliana na viongozi wa Taasisi hiyo namna ya kuboresha huduma za matibabu katika hospitali ya JKCI Dar Group wakati wajumbe wa Bodi hiyo walipotembelea Hospitali hiyo leo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu zinazotolewa.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu, baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo na viongozi wa JKCI wakiangalia maeneo malimbali ya Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo eneo la TAZARA jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari