Idara zilizotoa huduma bora kwa wateja zapongezwa


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kupitia taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo kwa mwezi Oktoba hadi Desemba 2022 kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akikabidhi cheti cha mshindi wa kwanza katika kutoa huduma bora kwa wateja kiongozi wa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) Afisa Muuguzi Lucia Kabeya wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Taasisi hiyo kupitia taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Kitengo cha ICU kimeongoza kwa kutoa huduma bora kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi cheti cha mshindi wa pili katika kutoa huduma bora kwa wateja Mkuu wa Idara ya Famasia Wellu Kaali wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Taasisi hiyo kupitia taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Idara ya Famasia imekuwa ya pili katika kutoa huduma bora kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2022.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akikabidhi cheti cha mshindi wa tatu katika kutoa huduma bora kwa wateja mwakilishi kutoka Maabara Emanuel Mgao wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Taasisi hiyo kupitia taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Idara ya Maabara imekuwa ya tatu katika kutoa huduma bora kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2022


Mratibu na msimamizi wa ubora wa huduma kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Adelphina Ncheye akiwasilisha taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa kikao cha wafanyakazi kupitia taarifa hiyo kwa mwezi Oktoba hadi Desemba 2022 jana katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Kitengo cha Huduma Bora kwa Wateja kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naiz Majani akielezea namna ambavyo kitengo hicho kimefanya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa kwa mwezi Oktoba hadi Desemba wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Taasisi hiyo kilichofanyika jana katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam.



Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia taarifa zilizokuwa zikitolewa wakati wa kikao cha kupitia taarifa ya ukaguzi wa ndani wa huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo kwa mwezi Oktoba hadi Desemba 2022 kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Picha na: JKCI

******************************************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari