Posts

Showing posts from 2024

JKCI yawapima moyo viongozi wa Taasisi za Umma

Image

Watoto 300 wafanyiwa upasuaji wa moyo kambi ya matibabu ya JKCI na Saudi Arabia

Image
Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahaya Ahmed Okeshi akizungumza na Rukia Ramadhani ambaye ni mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka  Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu cha nchini Saud Arabia wakati wa kufunga kambi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya watoto 30 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi hiyo. Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe.Yahaya Ahmed Okeshi akimpatia zawadi mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo Ester Benezed wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kw akushirikiana na wenzao wa Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu cha nchini Saudi Arabia. Jumla ya watoto 30 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi hiyo.  Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahaya Ahmed Okeshi akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.  Peter Kisenge alipo

Bima ya afya kwa wote itawapunguzia wananchi kulipia gharama kubwa za matibabu ya moyo

Image
  Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza mtoto Ally Mwandu aliyefanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumpatia ua la mkononi wakati alipowasili katika taasisi hiyo leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  na kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu cha nchini Saudi Arabia  alipotembelea JKCI leo kwaajili ya kuangalia  utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.   Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na ndugu wa wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati alipotembelea JKCI leo   JKCI leo kwaajili ya kuangalia  utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti m

Watoto 23 akiwemo wa umri wa siku tatu wafanyiwa upasuaji wa moyo

Image
Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia wakifanya upasuaji wa kurekebisha mishipa ya damu ya moyo wa mtoto ambayo haijakaa katika mpangilio wake wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo inayofanyika  JKCI. ********************************************************************************************************************************************************************************************************************** Na Stela Gama – JKCI Watoto 23 akiwemo wa umri wa siku tatu wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanyika katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).   Kambi hiyo maalumu ya upasuaji inafanywa na wataalamu wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao wa kituo cha Mfalme Salm

Kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa ya mishipa ya damu iliyotanuka (varicose vain) na ya artert kuziba

Image
  Wataalamu wa JKCI  wakimzibua mgonjwa mshipa wa damu ulioziba . *********************************************************************************************************************************************************************************************************************************************** Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inawaomba wataalamu wa afya kutoka Hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa nchini kuwatuma wagonjwa wenye matatizo ya kuziba kwa mishipa ya damu ili watibiwe  katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya kuzibua mishipa hiyo. Matibabu hayo yatakayotolewa tarehe 22 hadi 28 Septemba 2024 yatafanywa na   wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya   Andalusia ya nchini Misri. Matibabu yatakayotolewa katika kambi hiyo ni ya   kuzibua mishipa ya damu ya artery iliyoziba kwa kutumia mtambo wa Cathlab, upasuaji kwa njia ya kutumia matundu madogo katika kutibu mishipa ya damu ya vein iliyotanuka kwa kutumia kifaa cha umeme kijuli

JKCI na Saudi Arabia kufanya kambi ya upasuaji wa moyo kwa watoto

Image
Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nuru Letara na wenzake kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia Omar Almohyzy na Abdulrahman Eisa Redhyan wakijadiliana kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) wakati wa maandalizi ya kambi maalumu ya siku saba ya upasuaji wa moyo kwa watoto 30. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia Omar Almohyzy na mwenzake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nuru Letara wakiangalia majibu ya kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography – ECHO) mara baada ya kumpima mtoto wakati wa maandalizi ya kambi maalumu ya siku saba ya upasuaji wa moyo kwa watoto 30. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia Omar Almohzy akimfanyi

Uwekezaji mkubwa uliopo JKCI wawavutia wagonjwa kutoka nchi mbalimbali

Image

Rais Samia aipa JKCI Tuzo ya kutoa huduma za kipekee kwa jamii

Image

Viongozi washukuru kwa kupata huduma ya matibabu ya moyo katika kikao kazi cha Msajili wa Hazina

Image
Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka akimkabidhi Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina cheti cha shukrani ya kudhamini kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa taasisi za umma kwa kutoa huduma za upimaji, ushauri na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa washiriki wa mkutano huo uliomalizika hivi karibuni jijini Arusha. Afisa Muuguzi wa Hospitali ya AICC Loveness Swai akimpima shinikizo la damu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Maji Mbeya Neema Mwangwala wakati wa zoezi la upimaji afya ya moyo lililofanyika kwa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma walioshiriki kikao kazi cha siku tatu kilichomalizika hivi karibuni jijini Arusha. Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hamisi Msangi akimchukuwa vipimo vya damu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Tabora Anthony Mayunga kwaajili ya kumpima magonjwa mbalimbali wakati wa zoezi la upimaji afya ya moyo lililofanyi

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina tuzo ya taasisi ambayo imetoa  mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 tuzo hiyo ameitoa wakati  akifungua kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa Taasisi za umma kinachofanyika jijini Arusha. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Dkt. Angela Muhozya. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Angela Muhozya kabla ya kuwakabidhi  tuzo ya taasisi ambayo imetoa  mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024. Tuzo hiyo imetolewa leo jiji Arusha wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa Taas

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

Image
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Arusha kuhusu wataalamu wa Taasisi hiyo na wenzao wa hospitali ya AICC Arusha kutoa huduma za ushauri, upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wenyeviti na watendaji wakuu wa taasisi za umma watakaoshiriki kikao kazi kitakachofanyika jijini humo. Kikao kazi hicho cha siku tatu kimeandaliwa na ofisi ya Msajili wa Hazina. Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Arusha kuhusu wataalamu wa Taasisi hiyo na wenzao wa hospitali ya AICC Arusha kutoa huduma za ushauri, upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wenyeviti na watendaji wakuu wa taasisi za umma watakaoshiriki kikao kazi kitakachofanyika jijini humo. Kikao kazi hicho cha siku tatu kimeandaliwa na ofisi ya Msajili wa Hazina. Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya AICC Arusha Dkt. Ezekiel Moirana akizungumza na w

JKCI yatoa mafunzo kwa wauguzi kutoka nchini Zambia

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wauguzi kutoka nchini Zambia waliohitimu mafunzo ya miezi sita ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa na JKCI kwakushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo wakati wa hafla fupi ya kuwaaga jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpongeza Afisa Muuguzi kutoka nchini Zambia Christine Musonda aliyehitimu mafunzo ya miezi sita ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa na JKCI kwakushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKDI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na maafisa Uuguzi kutoa nchini Zambia waliohitimu mafunzo ya miezi sita ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa na JKCI kwakushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo wakati wa kuwaaga jijini