Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

Mwenyekiti wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tulizo Shem akizungumza na wanachama wa SACCOS hiyo wakati wa mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha JKCI akiwapongeza wanachama hao kwa kuweka jitihada za kuboresha mfuko wa SACCOS leo wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam

Afisa Ushirika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mihayo Malunde akielezea namna fedha zinazokusanywa na Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha JKCI zinaweza kuongeza uchumi wa wanachama wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wa SACCOS ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) uliofanyika leo katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam

Mjumbe wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magreth Mbarook akiuliza swali wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SACCOS hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Morris Obwanga akichangia mada wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SACCOS hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Flora Kasembe akiomba kupata ufafanuzi wa taarifa zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SACCOS hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Eng. Abella Rwiguza akichangia mada wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SACCOS hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.




Baadhi ya wanachama wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia taarifa zilizokuwa zikitolewa katika mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Na: JKCI

**************************************************************************************************

Wanawake wanachama wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (SACCOS) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaongoza kwa kumiliki hisa zenye thamani ya shilingi milioni 36.9 ukilinganisha na wanaume wanaomiliki hisa zenye thamani ya shilingi milioni 33.

Umiliki huo umechangiwa na idadi ya wanawake kuwa 190 sawa na asilimia 61 ukilinganisha na wanaume 151 sawa na asilimia 39 katika SACCOS,  hivyo kupelekea hisa kuongezeka na kuwa na thamani ya shilingi milioni 69.9 kutoka hisa zenye thamani ya shilingi milioni 4.8 mwaka 2020.

Akizungumza wakati wa mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge alisema kutokana na mafanikio ya SACCOS hiyo menejimenti ya Taasisi iliamua kutoa ofisi kwaajili ya uendeshaji wa shughuli za SACCOS ikiwa ni sehemu ya kuchangia ukuaji na maendeleo ya SACCOS.

Dkt. Kisenge amewataka viongozi wa SACCOS hiyo kuendelea kuzingatia sheria na weledi katika kuendesha shughuli za SACCOS ikiwa ni pamoja na kufanya kaguzi za hesaba, wanachama kupewa taarifa kwa wakati, kulinda haki za wanachama na kudumisha uwazi.

“Kumbukumbu zinaonyesha wazo la kuanzisha SACCOS hii lilipatikana mwaka 2019 na baadae 2020 kuzinduliwa na kuanza shughuli zake baada ya uongozi wa JKCI kuipa mtaji kama kianzio cha shilingi milioni 5 na leo tunaona SACCOS ina uwezo wa kukopesha zaidi ya shilingi milioni 30”, alisema Dkt. Kisenge

Dkt. Kisenge aliwataka viongozi wa SACCOS hiyo kuangalia namna ambavyo SACCOS inaweza kuongeza mapato yatakayosaidia kuongeza mikopo kwa wanachama ili wote kwapamoja waweze kufaidi matunda ya SACCOS hiyo.

Akitoa taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za SACCOS hiyo Mwenyekiti wa SACCOS ya JKCI Dkt. Tulizo Shem alisema kwa kipindi cha Januari 2024 hadi Novemba 2024 kiasi cha shilingi milioni 578 kimewekwa na wanachama 341 hivyo kufanya jumla ya akiba iliyowekwa kuwa shilingi bilioni 1.2.

“Jumla ya tozo zenye thamani ya shilingi milioni 35 zimekusanywa hadi Novemba 2024, ukifananisha na shilingi milioni 31 zilizokusanywa mwaka 2023 hivyo kuleta ongezeko la asilimia 12”, alisema Dkt. Tulizo Shem

Dkt. Shem alisema thamani ya mkopo kwa wanachama imeongezeka kutoka shilingi milioni 13 mwaka 2020 ikiwa ni mikopo 15 hadi kufikia shilingi bilioni 1.12 mwaka 2023 ikiwa ni mikopo 443.

Upande wa akiba za wanachama Dkt. Shem alisema akiba za wanachama zimeendelea kukua kutoka shilingi milioni 1.25 Januari 2020 hadi kufika shilingi milioni 580.3 Desemba 2023.

Aidha Dkt. Shemu alisema SACCOS hiyo inakabiiwa na changamoto ya uhitaji mkubwa wa mikopo kwa wananchama ukilinganisha na ukwasi uliopo pamoja na ukosefu wa elimu ya mifumo ya Tehama kwa wanachama.

Kwa upande wake mjumbe wa SACCOS hiyo Vedastus Lazaro amewaomba wafanyakazi ambao bado hawajajiunga na SACCOS hiyo kujiunga ili kuweza kutoa michango ya mwezi inayosaidia kuweka akiba itakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Vedastus alisema kupitia SACCOS hiyo ameweza kupata mkopo ambao aliutumia katika biashara zake pamoja na kuwasomesha wadogo zake kwani bila ya mkopo huo asingeweza kufanya hivyo.

Ziada Joram ambaye pia ni mjumbe wa SACCOS hiyo alisema SACCOS ya JKCI imemsaidia kuwekeza fedha ambazo kama zingekuwa kwenye akaunti yake angekuwa ameshazitumia.

Ziada alisema kupitia SACCOS hiyo ameweza kuchukua mkopo kwa urahisi na kwa wakati hivyo kuweza kufanya majukumu muhimu ya kifamilia.

“Kwakweli wafanyakazi ambao bado hawajajiunga na SACCOS hii wajiunge ili waweze kuwekeza na kukopa kwa maendeleo yao na taifa kwani SACCOS yetu ina riba ndogo ukifananisha na sehemu nyingine zinazotoa mikopo”, alisema Ziada

SACCOS ya wafanyakazi wa JKCI (JKCI SACCOS) ilianzishwa rasmi mwezi Agosti mwaka 2019 kwa Na. DSR. 1705 kwa kuzingatia sheria ya ushirika ya mwaka 2023 na kuanza majukumu yake Januari mwaka 2020.

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)