Posts

Showing posts from July, 2024

JKCI yapata tuzo katika kongamano la kisayansi nchini Kenya

Image
  Tafiti mbili kati ya tano za magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) zimechaguliwa kuwa tafiti bora na kupewa tuzo katika kongamano la kisayansi la 41 la mabingwa wa moyo nchini Kenya. Tafiti hizo mbili zilizopewa tuzo zilihusiana na utafiti wa ugonjwa wa moyo kutanuka kutokana na uzazi (Peripartum Cardiomyopathy) utafiti ambao umechukua miaka nane kufuatilia tatizo hilo. Akizungumza na mwandishi wa habari hii Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo alisema aliwasilisha tafiti hizo katika kongamano la kisayansi la 41 lililoandaliwa na chama cha madaktari bingwa wa moyo wa Kenya (Kenya Cardiac Society) na kufanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. “Tafiti mbili kutoka JKCI zilichaguliwa kuingia kwenye ushindani wa tafiti bora na kupewa tuzo, tafiti hizi zilihusiana na utafiti wa ugonjwa wa moyo kutanuka kutokana na uzazi (Peripartum Cardiomyopathy)”, alisema Dkt. Pedro Dkt. Pedro ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo al

Wananchi wa Wilaya ya Ilala wajitokeza kupima moyo

Image
Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Mahamoud Hassan akimpima wingi wa sukari kwenye damu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Sabina Zakaria akimpima shinikizo la damu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Said Sidde wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala. Naibu

Mtambo wa kuzalisha hewa ya oksijeni wenye thamani zaidi ya shilingi milioni 500 wazinduliwa Hospitali ya JKCI Dar Group

Image
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu akikata utepe wakati wa uzinduzi wa mtambo wa kuzalisha hewa ya oksijeni uliofanyika leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group. Mtambo huo hadi kusimikwa umegharimu shilingi milioni 526,604,116  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu akikagua eneo lililowekwa mtambo wa kuzalisha hewa ya oksijeni wakati akizundua mtambo huo leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group. Mtambo huo hadi kusimikwa umegharimu shilingi milioni 526,604,116 Mhandisi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abella Rwiguza akimuelezea Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu namna mtambo wa kuzalisha hewa ya oksijeni unavyofanya kazi wakati wa uzinduzi wa mtambo huo leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospi

Wanawake wa JKCI washirikiana katika matukio ya kijamii

Image
Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na mwenyekiti wa chama cha wanawake JKCI Dkt. Angela Muhozya wakimkaribisha Afisa Muuguzi mstaafu wa Taasisi hiyo Rehema Bakari wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Afisa Muuguzi Mstaafu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rehema Bakari akikata keki wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanywa na wanawake wa Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa chama cha wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Angela Muhozya akimkabidhi zawadi ya kitenge Afisa Muuguzi mstaafu wa JKCI Rehema Bakari wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Chama hicho pia kimempatia Bi. Rehema zawadi ya fedha taslim Tshs. 1,300,000. Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda akimpa kitenge cha pole ya kuondokewa na mzazi wake mfanyakazi wa JKCI Eng. Veronica Mugendi wakati wa kikao cha wanawake wa JKCI kilichofa

Watu 1,628 watibiwa moyo katika maonesho ya Sabasaba

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Suleiman Aboud Jumbe akimkabidhi tuzo ya mshindi wa pili kwa utoaji wa huduma za afya na matumizi ya teknolojia katika tiba Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda jana wakati wa kufunga maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara Dar es Salaam (Sabasaba). Baadhi ya washiriki wa maonesho ya sabasaba kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifurahia baada ya kupokea tuzo ya mshindi wa pili kwa utoaji  wa huduma za afya na matumizi ya teknolojia katika tiba wakati wa kufunga maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara Dar es Salaam. Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stanley Dickson akitoa elimu ya lishe bora kwa mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwaajili ya kupata huduma zinazotolewa wakati wa maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara Dar es Salaam yaliyomalizika jana katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Ki

JKCI yazindua kamati ya kusimamia masuala ya fedha endelevu

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati tendaji inayoshughulikia masuala endelevu ya fedha ya JKCI baada ya kuizundua leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Mwenyekiti wa kamati tendaji inayoshughulikia masuala endelevu ya fedha ya taasisi hiyo Mr. Iddi Lema adidu rejea za majukumu ya kamati hiyo leo wakati wa uzinduzi wa kamati hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni katibu wa kamati hiyo CPA. Agness Kuhenga Na: JKCI ****************************************************************************************************************

Wauguzi wapongenzwa kwa kutoa huduma bora

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na maafisa Uuguzi wanaosimamia vitengo mbalimbali vinavyofanya kazi za uuguzi baada ya kuwapatia vyeti vya kuthamini mchango wao katika kusimamia shughuli zinazofanywa na Taasisi. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo Aisha Omary cheti cha kuthamini mchango wake katika kusimamia shughuli zinazofanywa katika kliniki ya wagonjwa wa nje (POD) leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo anayesimamia wodi namba tatu Salama Mkinga cheti cha kuthamini mchango wake katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa wanaotibiwa na JKCI.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo anayesimamia katika wodi ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi

Watoto 300 wafaidika na matibabu ya moyo kupitia CRDB Marathon

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, viongozi wengine pamoja na watoto waliofanyiwa upasuaji wa moyo kupitia fedha za CRDB benki marathon wakati wa ufunguzi wa mbio hizo msimu wa tano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela akikabidhi bendera za nchi za Tanzania, Burundi na Congo kuashiria uzinduzi wa mbio za CRDB msimu wa tano zitakazofanyika katika nchi hizo mwezi wa nane mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI, matibabu ya akina mama wajawazito wenye mimba hatarishi na fistula pamoja na kuwezesha vijana kwa kuwajengea uwezo katika nyanja mbalimbali. Viongozi mbalimbali wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia hutuba zilizokuwa zikitolewa wakati wa ufunguzi wa mbio za CRDB benki marathon msimu wa tano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam Watoto walio

Viongozi mbalimbali wapongeza huduma zinazotolewa na JKCI katika banda la Sabasaba

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samwel George akimueleza Waziri wa afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui namna daktari aliyepo JKCI anaweza kusoma majibu ya mgonjwa anayetibiwa kwa kifaa maalumu kijulikanacho kwa jina la DOZEE kinachotumika kufuatilia maendeleo ya mgonjwa anayetibiwa akiwa nyumbani alipotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya Sabasaba. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Eben Ngowi akimpima urefu na uzito Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania Awadhi Juma Haji alipotembelea banda taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hassan Hafidh akimsikiliza Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hildegard Karau alipokuwa akimwelezea kuhusu huduma zinazotolewa katika banda la taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam Daktari wa Taasisi ya Moyo Jaka

Viongozi wa Serikali wavutiwa na huduma zinazotolewa na JKCI

Image

Huduma za kibingwa za matibabu ya moyo zafika Namtumbo

Image
Mbunge wa Jimbo la Namtumbo mkoani Ruvuma Mhe. Vitta Rashid Kawawa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu kambi maalumu ya siku sita ya uchunguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba itakayofanyika katika Wilaya ya Namtumbo kuanzia tarehe 8 hadi 13 mwezi Julai mwaka huu. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna huduma ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan itakavyofanyika katika Wilaya ya Namtumbo kuanzia tarehe 8 hadi 13 mwezi Julai mwaka huu wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mganga Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo na Mkuu wa Divisheni ya Afya, ustawi wa jamii na huduma za lishe Dkt. Aaron Hyera akielezea hali ya afya ilivyo kwa wananchi wa Namtumbo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya siku sita ya uchuguzi na matibabu ya moyo ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. S