Viongozi mbalimbali wapongeza huduma zinazotolewa na JKCI katika banda la Sabasaba
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samwel
George akimueleza Waziri wa afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Nassor
Ahmed Mazrui namna daktari aliyepo JKCI anaweza kusoma majibu ya mgonjwa
anayetibiwa kwa kifaa maalumu kijulikanacho kwa jina la DOZEE kinachotumika
kufuatilia maendeleo ya mgonjwa anayetibiwa akiwa nyumbani alipotembelea banda
la JKCI lililopo katika maonesho ya Sabasaba.
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Eben Ngowi akimpima urefu na uzito Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania Awadhi Juma Haji alipotembelea banda taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hassan Hafidh akimsikiliza Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hildegard Karau alipokuwa akimwelezea kuhusu huduma zinazotolewa katika banda la taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Nicole Kinyawa akimpima shinikizo la damu Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Mohamed Nyundo alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa maonesho ya sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam
Afisa Takwimu na Mafunzo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Makrina Komba akifanya mahojiano na raia wa Iran Monirch Sabagh aliyetembelea
katika banda la Taasisi hiyo lililopo katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea
katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
*******************************************************************************************************************
Viongozi mbalimbali wa Serikali wamepongeza huduma za
matibabu na elimu ya lishe zinazotolewa katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) lililopo katika maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara Dar es
Salaam.
Pongezi hizo zimetolewa leo wakati viongozi hao
walipotembelea banda la JKCI na kusema JKCI imeonyesha mabadiliko makubwa
katika kutoa huduma kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Akizungumza alipotembelea banda hilo Waziri wa Afya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui alisema JKCI kutumia huduma ya
afya mtandao kuweka miadi ya kuonana na daktari ni moja ya teknolojia ya kisasa
inayomsaidia mgonjwa kupata huduma za afya kwa wakati.
“Matumizi ya teknolojia katika Taasisi hii yanatumika vizuri
sana kwani mfumo wa huduma za afya mtandao unaotumika kwa wananchi kukutana na
wataalamu wa JKCI kupitia mtandao unatuwezesha kuzungumza na daktari tukiwa
mahali popote duniani”, alisema Mhe. Mazrui
Kwa upande wake Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la
Polisi Tanzania Awadhi Juma Haji aliwapongeza wataalamu wa JKCI kwa kutoa
huduma kwa wananchi katika maonesho ya Sabasaba.
Kamishna Haji alisema wananchi wanaposogezewa huduma karibu
uwapa nafasi kutumia muda huo kupima afya tofauti na kama wangeambiwa waifuate
huduma hiyo mahali zilipo hospitali.
“Nimetembelea banda hili na kupata elimu nzuri sana kuhusu
magonjwa ya moyo, wananchi wanaopenda kupata elimu sahihi kuhusu magonjwa haya
wasisite kutembelea banda la JKCI”, alisema Kamishina Haji
Naye Naibu Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe.
Hassan Hafidh aliupongeza uongozi wa JKCI kwa kuwa mstari wa mbele kutoa huduma
za kibingwa za matibabu ya moyo nchini.
Mhe. Hafidh alisema kutoa huduma za moyo katika maonesho ya
Sabasaba kunawapa fursa wananchi wengi kupima afya zao kwani maonesho hayo
yanatembelewa na wananchi wengi.
Comments
Post a Comment