Wauguzi wapongenzwa kwa kutoa huduma bora
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na maafisa Uuguzi wanaosimamia
vitengo mbalimbali vinavyofanya kazi za uuguzi baada ya kuwapatia vyeti vya
kuthamini mchango wao katika kusimamia shughuli zinazofanywa na Taasisi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo Aisha Omary cheti
cha kuthamini mchango wake katika kusimamia shughuli zinazofanywa katika
kliniki ya wagonjwa wa nje (POD) leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo anayesimamia wodi namba tatu Salama Mkinga cheti cha kuthamini mchango wake katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa wanaotibiwa na JKCI.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Afisa Muuguzi wa Taasisi hiyo anayesimamia
katika wodi ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (CCU) Tuzo Mcharo cheti
cha kuthamini mchango wake katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa wanaotibiwa
JKCI.
Comments
Post a Comment