Rais mstaafu Mhe. Dkt. Kikwete atembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete katika maonesho ya sabasaba


Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe.Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mahawa Asenga akimweleza kuhusu  huduma ya upimaji wa shinikizo la damu na kiwango cha sukari kwenye damu  anayoitoa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo lililopo katika maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe.Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaoshiriki katika maonesho ya sabasaba alipotembelea banda la taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Modesta Nyagawa akiwafundisha wananchi waliotembelea banda la taasisi hiyo namna ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wakati wa maonesho ya sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam.

                                               Picha na Hamisi Mussa

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari