Wananchi wa Wilaya ya Ilala wajitokeza kupima moyo

Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Mahamoud Hassan akimpima wingi wa sukari kwenye damu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Sabina Zakaria akimpima shinikizo la damu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Said Sidde wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Said Sidde wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu akizungumza na wananchi wa Ilala wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akielezea huduma zitakatotolewa wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo maalumu ya siku nne inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu

Wananchi wa Wilaya ya Ilala wakiendelea na huduma za vipimo wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika kwa siku nne katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu


Wananchi wa Wilaya ya Ilala na wilaya zingine wakiwa katika foleni ya kusubi huduma wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba inayofanyika kwa siku nne katika Zahanati ya Bungoni Kata ya Ilala jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo inafanywa na Hospitali ya JKCI Dar Group kwakushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu

Na: Stella Gama

********************************************************************************************************************

Wananchi wa Wilaya ya Ilala wametakiwa kujitokeza kwa wingi kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo katika kambi maalumu ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba.

Kambi hiyo maalumu iliyoanza leo inafanyika kwa siku nne katika Zahanati ya Bungoni iliyopo Kata ya Ilala kwa kutoa huduma bila gharama kwa wananchi wote watakaofika kwaajili ya kufanya vipimo vya magonjwa ya moyo, sukari, na shinikizo la damu.

Akizungumzia wakati wa ufunguzi wa kambi hiyo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kurahisisha huduma za matibabu na kuwafuata wananchi mahali walipo.

“Nawapongeza wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kufanikisha huduma hii ya upimaji kwa wananchi wa Wilaya ya Ilala, Matibabu ya moyo yana gharama kubwa lakini JKCI imetuletea hapa vifaa vya kisasa na mabingwa wa moyo ili waweze kutufanyia uchunguzi na kutupa ushauri, tutumie fursa hii kupima afya zetu”, alisema Mhe. Zungu

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu alisema JKCI imekuwa ikisogeza huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wananchi kuwapa fursa kupima afya zao kwani watu wengi hawana tabia ya kupima afya zao mara kwa mara.

“Tumekuwa tukipima afya zetu pale tunapoona changamoto za kiafya katika miili yetu lakini hatuna tabia ya kufanya uchunguzi kabla ya kuumwa ndio maana JKCI tumekuwa tukishirikiana na wadau mbalimbali kufikisha huduma za uchunguzi katika jamii kuijengea jamii yetu kuwa na tabia ya kuchunguza afya zetu mara kwa mara”, alisema Dkt. Shemu

Dkt. Shemu alimshukuru Mbunge wa Jimbo la Ilala kwa kuwakumbuka wananchi wa Ilala na kuwafikishia huduma hizo za kibingwa kwani kati yao wapo ambao wasingeweza kuzifuata mahali zilipo.

“Tunaishukuru sana ofisi ya Mbunge wa Ilala pamoja na wadau wengine kwa kuweza kushirikiana kwa pamoja kufanikisha huduma hii leo hapa Ilala, pia tunawashukuru wadau wetu kampuni za dawa ambao mmekuwa mkishirikiana nasi katika kambi zetu na kuwapatia wananchi dawa bila gharama”, alisema Dkt. Shemu

Naye mwananchi aliyejitokeza kwaajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya Thabia Mohamed alisema huduma za uchunguzi wa afya kupitia kambi hiyo zimewasaidia wananchi kuepuka gharama za matibabu kama wangezifuta hospitali.

Thabia aliomba huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo ziendelee kutolewa kwa karibu kwa wananchi ili ziweze kuwawezesha kupima afya zao na kuweza kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo.

“Baada ya kupata taarifa ya kambi hii ya matibabu wananchi wa Ilala tulikuwa na shahuku kubwa hatimaye leo imefika na tupo hapa toka asubuhi tunaendelea na huduma za vipimo vya moyo lakini pia tumepata elimu kuhusu magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo”, alisema Thabia


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari