Wanawake wa JKCI washirikiana katika matukio ya kijamii
Wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa
na mwenyekiti wa chama cha wanawake JKCI Dkt. Angela Muhozya wakimkaribisha Afisa
Muuguzi mstaafu wa Taasisi hiyo Rehema Bakari wakati wa hafla fupi ya kumuaga
iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa chama cha wanawake wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Angela Muhozya akimkabidhi zawadi ya kitenge Afisa Muuguzi mstaafu wa JKCI Rehema Bakari wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Chama hicho pia kimempatia Bi. Rehema zawadi ya fedha taslim Tshs. 1,300,000.
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda akimpa kitenge cha pole ya kuondokewa na mzazi wake mfanyakazi wa JKCI Eng. Veronica Mugendi wakati wa kikao cha wanawake wa JKCI kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
****************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment