Kwa mara ya kwanza abiria wanaosafiri na treni ya SGR kunufaika na huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari wakati wa
uzinduzi wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo itakayofanywa
kwa abiria wanaotumia treni ya SGR katika kuadhimisha siku ya moyo duniani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa
katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania
(TRC) Mhandisi Machibya Shiwa
wakati wa uzinduzi wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya
moyo itakayofanywa kwa abiria wanaotumia treni ya SGR katika kuadhimisha siku ya moyo duniani.
Picha na JKCI
*********************************************************************************** **********************************Kwa mara ya kwanza abiria wanaosafiri na treni ya
SGR kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonywa yasiyoambukiza yakiwemo
magonjwa ya moyo ndani ya treni.
Huduma hizo zitatolewa katika kambi maalumu
itakayofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) kwa
kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRC) ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya moyo duniani ambayo uadhimishwa kila
ifikapo tarehe 29 mwezi Septemba.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter
Kisenge alisema abiria watanufaika na uchunguzi huo bila malipo kuanzia tarehe
21 hadi 27 Septemba mwaka huu.
“Upimaji huo
utafanyika kwa kutumia mashine zinazotumia akili unde ambapo abiria watapimwa
kiwango cha sukari kwenye damu, uwiano wa uzito na urefu, shinikizo la damu
(BP), kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography -
ECHO) pamoja na kipimo cha kuangalia mfumo wa umeme wa moyo (Electocadiography-ECG)”,
alisema Dkt. Kisenge
Aidha Dkt. Kisenge aaliwataka wananchi na abiria kwa
ujumla kutumia fursa hiyo ya kipekee kupima afya zao ili wsweze kuepuka gharama
ambazo wangeweza kuzitumia kama wangefanyiwa vipimo hivyo Hospitalini.
“Kwa watu ambao wamekuwa wakisafiri mara kwa mara na
kukosa nafasi ya kufika katika vituo vya afya ni vema wakatumia fursa hii kwani
watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watapatiwa matibabu na wale
watakaohitaji majitabu zaidi tutawqpa rufaa ya kufika katika taasisi yetu
kwaajili ya uchunguzi zaidi”, alisema Dkt. Kisenge
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli
Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Shiwa
alisema abiria wengi watanufaika na zoezi hilo kutokana na idadi kubwa ya
wasafiri wanaohudumiwa na shirika hilo kwa siku.
“Abiria zaidi ya 12000 husafiri kila siku hivyo kupitia
kambi hii wananchi watanufaika na huduma za matibabu na kuweza kufahamu hali
zao za afya”, alisema Mha. Shiwa
Mhandisi
Shiwa alisema JKCI na TRC wana mpango wa kuwa na hospitali inayotembea katika
treni ya SGR, hii itasaidia kutoa huduma za dharura kwa wagonjwa
wanaosafirishwa umbali mrefu kwa kutumia magari ya wagonjwa (Ambulance).
Comments
Post a Comment