Tanzania, China zasaini mkataba wa ujenzi wa hospitali mpya ya JKCI Mloganzila
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe na Balozi
wa Jamhuri wa Watu wa China Mhe. Chen Mingjian wakionesha mkataba wa
utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI). Mkataba huo umesainiwa leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI iliyopo
jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe na Balozi
wa Jamhuri wa Watu wa China Mhe. Chen Mingjian wakisaini mkataba wa utekelezaji
wa ujenzi wa mradi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Mkataba
huo umesainiwa leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI iliyopo jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa
utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyopo
jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda akimkabidhi zawadi Katibu Mkuu wa
Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa
utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyopo
jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe, Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Chen Mingjian, Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge wafanyakazi na wataalamu wa afya kutoka Tanzania na china wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Picha Na
********************************************************************************************************************
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya
Afya na Jamhuri ya Watu wa China zimesaini Mkataba wa utekelezaji wa ujenzi wa
hospitali mpya ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) itakayojengwa Mloganzila.
Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam pamoja na
kufanya makabidhiano ya vifaa tiba na dawa kutoka kwa timu ya madaktari wa
Jamhuri ya Watu wa China ikiwa ni hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano wa
muda mrefu kati ya Tanzania na China katika sekta ya afya.
Akizungumza katika hafla hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya
Dkt. Grace Magembe alisema kusainiwa kwa mkataba huo ni ushahidi rasmi kwamba
mradi huo umeingia katika hatua mpya ya utekelezaji na uhusiano mzuri wa kidiplomasia kati ya
Tanzania na China unavyoendelea kuzaa matokeo yanayogusa moja kwa moja maisha
na ustawi wa watanzania.
“Upande wa sekta ya afya sisi tumekuwa wanufaika wakubwa sana
wa ushirikiano na Jamhiri ya Watu wa China. Moja ya matokeo yake ni Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambayo hapo nyuma hatukuwa nayo. Taasisi hii
tuliipata kutokana na ushirikiano ambao tumekuwa nao”, alisema Dkt. Magembe
Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania Chen Mingjian
alisema China imekuwa mshirika wa Tanzania katika sekta ya afya kwa muda mrefu
akitolea mfano JKCI ambayo ilikabidhiwa rasmi kwa Serikali ya Tanzania Septemba
2012 baada ya kujengwa kwa msaada wa China.
“Ninafurahi kuona kwamba baada ya zaidi ya muongo mmoja wa
maendeleo taasisi inaendelea kufanya vizuri. Wagonjwa wengi wa Tanzania
hawalazimiki tena kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya upasuaji wa moyo bali
wanaweza kupata huduma bora za matibabu hapa nchini kwa wakati”, alisema
Mingjian
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema ujenzi wa hospitali mpya ya JKCI utaunga
mkono mipango ya JKCI kuongeza huduma za kibingwa ikiwemo mpango wa kuanza
kutoa huduma za upandikizaji wa moyo (heart transplant) ifikapo mwaka 2030.
“Mradi huu ni matokeo ya ushirikiano mzuri unaofanywa na
Tanzania na China ambao ulianza tangu miaka ya sitini. Hospitali itakayojengwa
itakuwa na teknolojia ya hali ya juu na itaifanya JKCI kuwa kituo kikubwa cha
matibabu na upasuaji wa moyo kwa Afrika Mashariki na Kati”, alisema Dkt.
Kisenge.
Ujenzi wa Hospitali mpya ya moyo nchini unatarajiwa kuongeza
uwezo wa Tanzania katika kutoa huduma bingwa na za kisasa za uchunguzi na
matibabu ya moyo pamoja na kuimarisha utaalamu, teknolojia na miundombinu ya
huduma za moyo nchini.
Comments
Post a Comment