Mamia wajitokeza kupima moyo Kilimanjaro
Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro na mikoa ya jirani
wakisubiria kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo katika Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa Mawenzi (MRRH) wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya
moyo inayofanywa na wataalamu wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa MRRH.
Afisa
Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magdalena Chikawe akimpima
sukari kwenye damu mwananchi aliyefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
Mawenzi (MRRH) wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo
inayofanywa na wataalamu wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa MRRH.
Daktari
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Magreth Ng’ondya na mwenzake kutoka
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi (MRRH) Benson Towo wakimsikiliza mwananchi
aliyefika katika Hospitali hiyo kwaajili ya kufanyiwa vipimo vya moyo wakati wa
kambi maaalum ya siku tano ya upimaji na matibabu ya moyo inayofanywa na
wataalamu wa afya kutoka JKCI na wenzao wa MRRH.
Afisa lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna
Faraji na mwenzake kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi Ester Wazoel
wakimpatia ushauri wa lishe mkazi wa Kilimanjaro aliyefika katika Hospitali hiyo
kwaajili ya kupima moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayofanywa na
wataalamu wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa MRRH.
****************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment