JKCI wamuaga Prof. Mahalu
Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisukuma toroli lililobeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu ambaye pia alikuwa daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wakielekea kwenye ibada ya kumuaga iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wanataaluma ya afya wakiwa katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimfariji mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu wakati wa ibada ya kumuaga iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.
Picha na Khamis Mussa
Comments
Post a Comment