JKCI wamuaga Prof. Mahalu

Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisukuma toroli lililobeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu ambaye pia alikuwa daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wakielekea kwenye ibada ya kumuaga iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.

Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wanataaluma ya afya wakiwa katika ibada ya kumuaga  aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimfariji mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Marehemu Prof. William Mahalu wakati wa ibada ya kumuaga iliyofanyika leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Muhimbili.

Picha na Khamis Mussa


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari