Wafanyakazi bora watunukiwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi tuzo Afisa Muuguzi mstaafu wa Taasisi hiyo Mary
Haule wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2022/2023
aliyeshika nafasi ya kwanza afisa Uuguzi Samweli mpiga akipokea ngao ya mfanyakazi
bora kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao
iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar
es Salaam.
Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2022/2023
aliyeshika nafasi ya pili Fundi Sanifu wa Moyo Jasmine Keria akipokea cheti cha
mfanyakazi bora kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi
hao iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini
Dar es Salaam.
Mfanyakazi bora wa robo ya nne ya mwaka wa fedha 2022/2023
aliyeshika nafasi ya tatu Radiografa wa JKCI Shaniath Mziray akipokea cheti
cha mfanyakazi bora kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi
hao iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini
Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
******************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment