Wapewa mafunzo ya kutambua viashiria vya hatari katika utendaji kazi


Mkufunzi kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Dkt. Indiael Kaaya akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika hivi karibuni.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Martin Rubamba akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa JKCI hivi karibuni.

Mteknolojia wa Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mariam Steven akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo hivi karibuni.

Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti na Ubora wa Huduma wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizhijwa Majani akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo mara baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku mbili ya namna ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa JKCI.

Picha na: JKCI

******************************************************************************************************************

Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamepewa mafunzo ya siku mbili ya kutambua viashiria mbalimbali vinavyoweza kusababisha hatari katika utendaji wa kazi vinavyoweza kujitokeza katika mazingira na sura mbalimbali.

Mafunzo hayo ambayo yatatolewa kwa wafanyakazi wote wa Taasisi hiyo yameanza kutolewa kwa wafanyakazi 50 ambao ni risk champions katika maeneo yao ya kazi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti wa Ubora wa Huduma wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Dkt. Naizhijwa Majani alisema mafunzo hayo ambayo ni yakwanza kufanyika yametolewa kwa kundi la kwanza la wafanyakazi 50 ambapo baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo wafanyakazi wote watapewa muongozo wa namna bora ya kudhibiti vihatarishi katika Taasisi hiyo.

 “Nia yetu kubwa ni kuhakikisha wagonjwa wetu, wafanyakazi wa JKCI na wageni wote wanaofika katika Taasisi yetu wanakuwa salama wakati wote”, alisema Dkt. Naizhijwa

Dkt. Naizhijwa alisema JKCI ina maono ya kuwa Taasisi ya kimataifa katika kutoa huduma za kibingwa za uchunguzi na matibabu ya moyo nchini pamoja nchi zilizopo barani Afrika hivyo ni muhimu kukabiliana na vihatarishi vinavyoweza kukwamisha Taasisi kufikia malengo yake.

“Ili tuweze kuwa katika viwango vya juu vya kutoa huduma za matibabu ya moyo kimataifa lazima tuwe imara na kuweka mifumo ambayo itatusaidia kujiandaa kukabiliana na vihatarishi vinavyoweza kujitokeza”, alisema Dkt. Naizhijwa

Kwa upande wake mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Dkt. Indiael Kaaya alisema msingi wa mafunzo ya udhibiti wa vihatarishi hujengwa ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia malengo ya Taasisi.

Dkt. Kaaya ambaye pia ni mshauri na mtafiti alisema mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kujipanga na kuona uwepo wa kesho leo ili waweze kutafakari yale ambayo wamekuwa wakifanya katika Taasisi hiyo na kuweka mikakati ya kudhibiti vihatarishi kabla ya kutokea.

“Katika mafunzo haya tumepitia miongozo mbalimbali inayotutaka kusimamia vihatarishi katika Taasisi za umma pamoja na kuangalia mifumo rasmi inayosimamia udhibiti wa vihatarishi”, alisema Dkt. Kaaya

Dkt. Kaaya alisema mfumo wa usimamizi wa kudhibiti vihatarisha unatoa muongozo wa namna ya kung’amua vihatarishi na kuunganisha mpango wa udhibiti vihatarishi na mpango wa Taasisi kwa ujumla.

Naye mshiriki wa mafunzo hayo ambaye ni Mtaalamu wa Tiba Mionzi katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Amani Materu alisema kupitia mafunzo hayo ameweza kujifunza vitu vingi ikiwemo kutambua na kudhibiti vihatarishi endapo vitatokea katika eneo lake la kazi.

Materu alisema upande wake kama mtaalamu wa tiba mionzi ameweza kuainisha vihatarishi vinavyoweza kumrudisha nyuma katika utendaji wake wa kazi kama hatazua vihatarishi vinavyoweza kujitokeza katika kazi zake za kila siku.

“Kitu kikubwa kinachoweza kukwamisha malengo katika eneo langu la kazi ni kuharibika kwa mashine, kutokea kwa hitilafu za umeme na mifumo ya utumaji wa majibu ya mgonjwa, kwa kutambua vyanzo hivyo tutaenda kuchukua hatua za mapema ili kukabiliana na vihatarishi vinavyoweza kujitokeza”, alisema Materu

Materu alisema mafunzo hayo yanaenda kuwa rafiki katika eneo lake la kazi lakini pia kumsaidia hata nje ya eneo la kazi ikiwemo katika familia yake pamoja na jamii iliyomzunguka.

Mafunzo hayo kwa awamu ya pili yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba ambapo wafanyakazi 200 wa JKCI watashiriki na awamu ya tatu yatafanyika mwakani Januari ambapo wafanyakazi wengine 200 watashiriki.

 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari